LICHA YA UZURI WAKE MWANADADA ELIZABETH MICHAEL a.k.a LULU SI MALI KITU MBELE YA RAY, AMKWEPA KUOGOPA AIBU.



Elizabeth Michael ‘Lulu’. 

STAA wa filamu Bongo, Vincent Kigosi ‘Ray’ amesema alipata wakati mgumu kumpanga mwigizaji Elizabeth Michael ‘Lulu’ kwenye filamu yake ambayo walipaswa kucheza kama wapenzi kwa kuhofia kumbusu.


Akizungumza katika kituo kimoja cha runinga cha jijini Dar hivi karibuni, Ray alisema licha ya kuwa Lulu alikuwa anastahili kuigiza katika sinema ya Woman Principle miaka kadhaa iliyopita, aliona Lulu anafaa kutokana na umakini wake lakini akaona bora amchukue Miss Tanzania namba 3, 2003, Nargis Mohammed kwa kuhofia kupata aibu ya kuoneshana malavidavi na Lulu.

 
 Vincent Kigosi ‘Ray’.

“Lulu alikuwa na uwezo wa kumudu kipengele hicho, kipindi hicho alikuwa mdogo sana, niliona ni jambo la aibu kidogo kumbusu mdomoni mtoto mdogo kama yeye halafu ni kitu ambacho jamii itakaa ikitazame nikaona bora nimchukue Nagris, Lulu nikampa sini nyingine,” alisema Ray.

Aliongeza kuwa, kikubwa kilichomfanya avutiwe kucheza na Nagris ni kwa sababu ni mwanamke ambaye katulia na hana skendo hivyo itamuongezea heshima na mvuto wa kazi yake katika jamii.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

𝙂𝘼𝙈𝙊𝙉𝘿𝙄 𝙆𝘼𝘾𝙃𝙀𝙕𝘼 𝙆𝙄𝘽𝙄𝙉𝙂𝙒𝘼.