BAYERN YAIFUNGASHA VIRAGO MAN UTD, BARCA YACHEZEA KWA ATLETICO.


Usiku wa jana haukuwa mzuri kabisa kwa meneja wa mashetani wekundi ‘David Moyes’ baada ya kikosi chake  kukubali kipigo cha bao 3 – 1 kutoka kwa wenyeji wao,  timu ya Bayern Munich ya Ujerumani.
EvraBeki wa Manchester United, Patrice Evra akishangilia bao lake la kwanza.
United ndio waliotangulia kupata goli la kwanza   kupitia beki wake ‘Patrice Evra’ mnamo dakika ya 57′ ya  kipindi cha pili cha mchezo.
Moyes DHapa ni ule wakati wa benchi la ufundi la United wakiongozwa na kocha Moyes wakishangilia bao la kwanza alilofunga Evra. kweli kutangulia sio kufika.
Hata hivyo hali ya mchezo ilibadilika ghafla baada ya mshambuliaji wa Munich ‘Mario Mandzukic’  kusawazisha  dakika ya 59′ na kisha kufuatiwa na Thomas Muller aliyefunga goli la pili dk 68′ kabla ya kijana mzee ‘Arjen Robben’ kufunga bao la tatu dakika ya 76 na kuifanya timu yake kufuzu hatua ya nusu fainali.
Robben

Ribery akimpongeza Arjen Robben baada ya kupachik.a bao la tatu
SimanziFuraha ilipofikia mwisho wake, Kocha wa United ‘Moyes’ akifuta machozi huku akishuhudia vijana wake wakisulubiwa goli 3 na wajerumani.
Mchezo mwingine uliokuwa wa patashika nguo kuchanika ni ule uliozikutanisha timu mbili za hispania,  Atletico Madrid na Barcelona, ambao ulimalizika kwa Atletico kuibuka na ushindi wa bao 1 – 0 dhidi ya Barca kupitia mchezaji wao  Koku dakika ya 5 na hivyo kujitwalia jumla ya pointi 6 na  magoli 3 – 1 dhidi ya Barcelona katika michezo miwili waliyocheza na kufuzu hatua ya nusu fainali.
Koke wa Atletico akishangilia bao lake baada ya kumzidi ujanja kipa wa Barca.
Koke wa Atletico akishangilia goli alilowafunga Barcelona.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*