Mlipuko
mkubwa umetokea hapo jana majira ya saa 1.30 usiku katika baa maarufu
ya Arusha night park iliyopo eneo la Mianzini mjini Arusha na kujeruhi
watu waliokuwepo eneo hilo.
Taarifa za awali zinaeleza kuwa
mlipuko huo ulitokana na bomu lililotengwa katika eneo la bar hiyo na
kujeruhi watu zaidi ya 20 waliokuwa wakiangalia mechi kati ya Chelsea na
Swansea.
Majeruhi wamekimbizwa katika
hospitali ya dk. Mohamed na Mount Meru. Mashuhuda wanaeleza kuwa kuna
baadhi ya majeruhi wamekatika viungo kama miguu nakadhalika.
Hili ni tukio la tatu mjini arusha
bomu kurushwa na kutegwa katika maeneo ya mikusanyiko ya watu ambayo
ilipelekea kujeruhi na kupoteza maisha ya watu.
Comments