Naibu
Waziri wa Afya Zanzibar Dokta Sira Ubwa Mamboya akimkaribisha Makamu wa
Pili wa Rais Balozi Seif Ali Iddi katika uzinduzi wa kampeni za kutoa
huduma za kisukari na shinikizo la damu zitakazofanyika Mikoa yote ya
Zanzibar.
Mratibu
wa mtadi wa kutoa huduma za kisukari na shinikizo la damu Mr. Siraji M.
Mtulia akitoa maelezo mafupi ya mradi huo utakaoanza kutekelezwa leo na
Chama cha wanafunzi Madaktari Tanzania wakishikiana na Wizara ya Afya
Zanzibar.
Mkuu
wa CHUO cha (IMTU) Prof. Flora Fabian akitoa maelezo kuhusu madaktari
hao walivyojipanga kufanya kazi katika Mikoa yote ya Unguja na Pemba.
Makamu
wa Pili wa Rais Balozi. Seif Ali Iddi akiwahutubia Madaktari na
wananchi waliofika katika uzinduzi wa kampeni za kutoa huduma za
kisukari na shindikizo la damu huko ukumbi wa Chuo Kikuu cha Taifa Suza
Mjini Zanzibar.
Balozi Seif na Naibu Waziri wa Afya Dkt. Sira wakikagua utoaji huduma mara baada ya kuzindua.
Makamu
wa Pili wa Rais Balozi. Seif Ali Iddi (wakatikati waliokaa) katika
picha ya pamoja na wanafunzi madaktari kutoka vyuo mbalimbali Tanzania.
Balozi Seif akiagana na wanafunzi madaktari mara baada ya kuzindua huduma za upimaji afya katika sherehe zilizofanyika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Taifa Suza Mjini Zanzibar. PICHA ZOTE NA MAKAME
MSHENGA WA MAELEZO ZANZIBAR.
Comments