Mwanamuziki Diamond Platnumz ameandika leo kupitia ukurasa
wake wa Facebook akiwashukuru watanzania na wapenzi wa muziki wake
wanaoendelea kumpigia kura kwa ajili ya kumuwezesha kunyakua tuzo kubwa
za Afrika ‘KORA’ ambazo hufanyika mara moja kwa mwaka.
Tuzo hizo zinawapa nafasi mashabiki ya kuwapigia kura kwa njia ya
mtandao wasanii wanaowaona wanastahili kushinda kwa njia ya kulike
ukurasa wa Kora kisha kulike katika kila posti utakayoona picha au jina
la msanii unayemkubali.
Wiki hii Diamond ameweza kupata kura zilizoweza kumtoa nafasi
ya 14 wiki iliyopita mpaka nafasi ya tatu kwa wiki hii ikiwa ni kwa
Afrika nzima. Amr Diab, Koffi Olomide, Fally Ipupa, Werrason,
Mafikizolo ni baadhi ya wasanii waliopo kwenye kinyang’anyiro kimoja na
rais wa watu wasafi ‘Diamond’.
”Hakika nimeamini Umoja ni nguvu, na tukizidi kushirikiana mziki wetu utazidi fika mbali na kuleta heshima na sifa zaidi nyumbani… Kutoka nafasi ya 14 katika tunzo za Kora wiki ilopita hadi leo kushika nafasi ya 3 Africa Nzima… kiukweli ni hatua kubwa sana, na nawashkuru sana sana… tafadhari naomba kwapamoja mnipigie kura tena na hatimaye tushike nafas ya kwanza na hadi kutwaa kabisa….JINSI YA KUPIGA KURA: unaingia katika link hii hapo chini kisha unalike page ya Kora Awards kisha katika kila Post utayoona jina au Picha yangu Unacomment kwa kuandika Jina langu Diamond Platnumz… hapo utakuwa umeniwezesha… kama ushalike page usiilike tena, Ahsante!” Aliandika Diamond…
Unaweza ukashiriki kumpigia kura kwa kubofya Link hapo >>> https://m.facebook.com/photo.php?fbid=373823212756836&id=355750224564135&set=a.355773297895161.1073741831.355750224564135&source=46
Comments