Mwanamuziki
nguli wa muziki wa kufokofoka nchini Tanzania, Godfrey Tumaini
‘Dudubaya’ amekanusha vikali tuhuma zinaendelea kusambaa kama moto wa
kifuu kuhusu kumkata sikio mama yake mkubwa huku akidai kwamba
wanaosambaza maneno hayo ni ndugu zake wa damu kabisa ambao wanamuonea
wivu kufuatia kitendo chake cha kumjengea nyumba mama yake mzazi.
”Nashangaa sijapigiwa simu na sijua kama kuna tukio gani ama
nini. Unajua hivi vitu sivielewi, mimi nawasiwasi hii inshu na ndugu
zangu binafsi. Ndugu zangu walikuwa wakiongea maneno kibao mara Dudubaya
hajajenga kwao kisesa. Kwa hiyo ni ndugu ambao hata kwenye hili suala
wanajaribu kukrieti vitu flani kwamba huyu kafanya hivi kumkata sikio
mama yake mkubwa ili kunichafulia katika jamii nionekana namna gani”
alisema Dudubaya alipokuwa akifanyiwa mahojiano na Soudy Brown ‘Gossip
Cop’.
Comments