JERRY SILAA AGAWA DAWATI 300 KWA SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA ILALA


DSC_0546
Mwenyekiti wa huduma za jamii manispaa ya Ilala, Angelina Nyalembeka akitoa ufafanuzi kuhusiana na kero za wadudu aina ya Kunguni katika shule hiyo ambapo amesema mwaka jana walipulizia dawa kwenye mabweni yote ya wanafunzi na haraka iwezekanavyo ataliwasilisha kero hiyo kwenye vikao vya Manispaa na kupatiwa ufumbuzi na wanafunzi waweza kukaa kwa amani bila usumbufu.
DSC_0572
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala ambaye pia ni Diwani wa kata ya Gongo la Mboto, Jerry Silaa, akizungumza na waalimu pamoja na wanafunzi wa shule ya Sekondari Pugu, kabla ya kukabidhi madawati kwenye hafla fupi iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
DSC_0527
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya Sekondari Pugu wakifuatilia risala ya mgeni rasmi Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa.
DSC_0622
Mstahiki Meya Jerry Silaa akiteta jambo na mmoja wa wanafunzi wa kidato cha tatu ambaye ni mlemavu Voster Peter wakati akikabidhi madawati shuleni hapo.
DSC_0482
Baadhi ya viongozi wa Kata ya Pugu, Gongo la Mboto na Upanga Magharibi waliohdhuria hafla hiyo.
DSC_0626
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa akifurahi jambo na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Pugu, Jovinus Mutabuzi, wakati hafla fupi ya kukabidhi madawati 107 kwa shule hiyo. Kushoto ni Mwenyekiti wa huduma za jamii manispaa ya Ilala, Angelina Nyalembeka akifuatiwa na Diwani wa Kata ya Pugu, Imelda Samjela.
DSC_0631
Sasa mtajinafasi wakati wa masomo darasani si ndio..? Mstahiki Meya Jerry Silaa akimuuliza mmoja wa wanafunzi wa shule ya sekondari Pugu alipokuwa akikabidhi madawati.
DSC_0638
Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Ulongoni, Bi. Sikitiko Salehe,( wa pili kulia) akipokea moja ya madawati kati ya 93 kwa niaba ya shule yake kutoka kwa Mstahiki Meya Jerry Silaa ikiwa ni zao la matunda ya Mayor's Ball 2013 iliyoweka kipaumbele kwenye elimu kuhakikisha kila mwanafunzi anakaa kwenye dawati katika hafla fupi iliyofanyika kwenye shule ya sekondari Pugu jijini Dar.
DSC_0645
Wanafunzi wa Shule ya sekondari Pugu wakionyesha nyuso za furaha isiyo na kifani walipokabidhiwa madawati 107 na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa.
DSC_0661
Mstahiki Meya Jerry Silaa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa ngazi mbalimbali Kata za Gongo la Mboto na Pugu.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI