KATIBU MKUU WA CCM,KINANA ATEMBELEA MJI WA KIHISTORIA WA UJIJI,AKUTANA NA WAVUVI WADOGO WADOGO ZIWA TANGANYIKA
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akipata maelezo mafupi ndani ya Nyumba ya Makumbusho ya Dr Livingstone iliyopo katika eneo la Ujiji mkoani Kigoma
Katibu
Mkuu wa CCM (tatu kulia),Ndugu Kinana pamoja na viongozi mbalimbali wa
CCM,Mkoa na Wilaya wakipata maelezo mafupi kuhusiana na historia ya
mnara huo,ambao Dr.Livingstone na Henry M.Stanley walikutana kwa mara ya
kwanza katika mji wa Kihistoria wa Ujiji mkoani Kigoma katika suala
zima la kusambaza dini na kupambana na biashara ya Utumwa.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mama Mawazo Rashid Mawala
mkazi wa Ujiji Kigoma ,Katibu Mkuu alikuwa akitembea kwenye njia (route) iliyotumika na
Watumwa ambapo kuna miembe yenye umri zaidi ya miaka 150,miembe kama hii inapatikana sehemu ya ya Tabora na Bagamoyo.
Sehemu
ya njia (route) kama ionekanavyo pichani ndani mji wa kihistoria Ujiji
mkoani Kigoma,iliyotumika kusafirishia Watumwa kwenda sehemu
mbalimbali,katika njia hiyo kuna miembe inayoelezwa ina umri zaidi ya
miaka 150 tangu kupandwa kwake,na inaelezwa inapatikana sehemu ya Tabaro
na Bagamoyo.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimsikiliza Mzee Masoud Mwinyi
Chande kwenye mnara wa kumbukumbu ya nyumba ya kwanza ambayo Mwalimu
Julius Nyerere alifikia Ujiji wakati akifanya harakati za kutafuta
Uhuru, Inaelezwa kuwa Nyumba hiyo Mwalimu Nyerere alifika akiongozana na
Suleiman Takadili na Bibi Titi Mohamed.Kulia ni Mbunge wa Kigoma
Mjini,Mh Peter Serukamba,Katibu wa NEC,Siasa na Uenezi,Nape
Nnauye,pamoja na Mwenyekiti wa CCM-Kigoma Ndugu Amani Kabouru.
Katibu
Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akielekezwa sehemu ya Chumba na mlango ndani
ya nyumba ya kwanza ambayo Mwalimu Julius Nyerere alifikia Ujiji wakati
akifanya harakati za kutafuta Uhuru, Nyumba hiyo inasemekana Mwalimu
Nyerere alifika akiongozana na Suleiman Takadili na Bibi Titi Mohamed.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana na viongozi mbalimbali wa CCM Wilaya na Mkoa,wakiwasilia kwenye Nyumba ya Makumbusho ya Dr Livingstone iliyopo katika eneo la Ujiji mkoani Kigoma na kujionea mambo mbalimbali ya kihistoria yaliyomo ndani ya jengo hilo.
Mmoja
wa wakazi wa eneo la Kibiri,ambalo liko ufukweni kabisa mwa ziwa
Tanganyika mkoani Kigoma,akibandika mabango yake yenye ujumbe wa
kumpokea Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana,alipokwenda kutembelea eneo
hilo na kusikiliza kero mbalimbali za wavuvi wadogo wadogo.
Baadhi
akina Mama ambao ni wafanyabiasha wa samaki na dakaa pamoja na uvuvi
wakiwa wamekusanyika wakimsubiri Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana kwa
ajili ya kuwazisilisha kero zao mbalimbali ikiwemo tozo za kodi na
ushuru mkubwa ikilinganishwa na kipato chao.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisoma bango
lenye ujumbe wa kulalamikia kodi kubwa
wanazotozwa wavuvi wadogowadogo wa Kibirizi,Kigoma.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia
wakazi wa Kibirizi mkoani Kigoma ambao wanakilio cha kutozwa kodi kubwa,
kuvamiwa na majambazi wakati wa shughuli zao za uvuvi.
Katibu Mkuu,Ndugu Kinana akikata utepe kuashiria ufunguzi wa Ofisi mpya ya CCM,kata ya KIbirizi.
Katibu
Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akizungumza kwenye kikao cha Mabaraza ya
Jumuiya zote (CCM) katika ukumbi wa Kibo Peak Club,Wilaya ya Kigoma
mjini mkoani humo,ambapo Kinana walizungumza mambo mbalimbali ya
kutekeleza na kuhimiza Ilani ya uchaguzi ya mwaka 2010,pamoja na miradi
mbalimbali ya maendeleo ya jamii.
Pichani
Kati ni Mbunge wa Kigoma Mjini,Mh Peter Serukamba akieleza jambo kwa
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana (shoto) wakati wakielekea kutazama Nyumba ya Makumbusho ya Dr Livingstone iliyopo katika eneo la Ujiji mkoani Kigoma,kulia ni a Katibu wa NEC,Siasa na Uenezi,Nape Nnauye.
Comments