KIPINDI KIPYA: SIKILIZA LIVE KUTOKA SOKO LA HABARI KARIAKOO...!


Leo Jumatatu, Aprili 7, Redio yako ya Kijamii ya KwanzaJamii imeandika historia kwa kuwa redio ya kwanza hapa nchini kuwaletea wasikilizaji dondoo za habari za magazetini kutokea kwenye soko lenyewe la habari, ni  pale kona ya Uhuru na Msimbazi, Kariakoo.

Ni kipindi cha kila siku kuanzia saa kumi na moja na nusu alfajiri. Mwandishi/ Mtangazaji wa KwanzaJamii atakuwa sokoni hapo na kuungana moja kwa moja na studio za Kwanzajamii radio Iringa.

Sambamba na redio, habari hizo na picha za magazeti yenyewe zitarushwa pia kwenye Mjengwablog.com. Ikumbukwe, Mjengwablog ilikuwa ni blogu ya kwanza hapa nchini kuanza kurusha kwenye blogu dondoo za magazetini.

Usikose kufuatilia na kuzipata habari zikiwa motomoto kutoka Soko la habari Kariakoo...http://www.mjengwablog.com/habari-za-kijamii/item/10489-kutoka-soko-la-habari-kariakoo.html#.U0JH6ldQ7U4

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA