MACHANGUDOA WAWASIFIA BAADHI YA WABUNGE WANAUME WA BUNGE LA KATIBA KWA KUTOA KITITA KIZURI MARA BAADA YA KUKUBALIANA NAO KWA AJILI YA KUFANYA NAO MAPENZI MJINI DODOMA.


Wasichana wanaofanya biashara ya kujiuza katika maeneo mbalimbali mjini hapa wameelezea neema iliyowafikia kufuatia kujikusanyia pesa ndefu kutoka kwa baadhi ya wabunge wa Bunge la Katiba ambao wanadaiwa kuwalipa vizuri.Wakizungumza na Ijumaa kwa nyakati tofauti, wadada hao ambao baadhi wanatokea Mikoa ya Dar, Arusha, Mbeya na kwingineko walisema kipindi hiki wanakiita ni cha mavuno kwao kwani waheshimiwa hao si watu wa kulipa pesa ndogo wanapowaopoa.

“Yaani sasa hivi ni kipindi cha mavuno, wateja ni wengi na wanalipa vizuri tofauti na kipindi cha nyuma. Kwa mfano ukibahatika kumpata mjumbe wa bunge hili linaloendelea sasa, mbona utafurahi na roho yako! Wanalipa vizuri ile mbaya.

“Kipindi cha nyuma unaweza kulala na mtu akakulipa shilingi 30,000 au 20,000 lakini sasa hivi ni 50,000 kwenda juu, hakuna longolongo, tusipojenga safari hii basi tena,” alisema msichana mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Husna ambaye kiwanja chake kikuu cha biashara ni eneo Chako ni Chako.

Mwingine ambaye aliomba jina lake lisiandikwe gazetini akidai yuko Dodoma bila ndugu zake walioko Dar kujua alisema: “Unajua hii biashara inakuwaga na usumbufu sana, unaweza kuchukuliwa na mtu asikulipe lakini sasa hivi wateja wetu wakuu ni hawa wabunge, wengine wametugeuza nyumba ndogo zao kabisa.”

Hata hivyo, uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa, biashara hiyo sasa imeshika kasi kiasi kwamba baadhi ya waheshimiwa humalizia posho zao za siku kwa kuzitumbua na madadapoa hao.

Mwandishi wetu alifanya doria siku za wikiendi maeneo ya Chako ni Chako, Mwenga Bar na zaidi katika kumbi za starehe kama vile Club 84 na Maisha na kushuhudia magari yakipaki na kupakiza wasichana kisha kuondoka.

Gazeti hili linatumia nafasi hii kuwaasa waheshimiwa kufanya walichokifuata bungeni na kuacha michepuko isiyokuwa na maana na wale wasichana walioona njia sahihi ya kutafuta maisha bora ni kwa kujiuza, wajue kufanya

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

𝙂𝘼𝙈𝙊𝙉𝘿𝙄 𝙆𝘼𝘾𝙃𝙀𝙕𝘼 𝙆𝙄𝘽𝙄𝙉𝙂𝙒𝘼.

DK NCHIMBI ATINGA MKOANI KATAVI