MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA KONGAMANO LA 28 LA MWAKA LA NIMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia wakati akizindua rasmi Kongamano
la 28 la Mwaka la Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Tiba (NIMR). Kongamano
hilo lililofanyika kwenye Ukumbi wa Mwalimu Nyerere, jijini Dar es
Salaam, limeandaliwa na Taasisi hiyo ya (NIMR).
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akikata utepe kuashiri kuzindua Mpango wa Mkakati wa Nne wa Utafiti
Bora wa Afya, wakati wa ufunguzi wa Kongamano la 28 la Mwaka la Taasisi
ya Taifa ya Utafiti wa Tiba (NIMR), lililofanyika kwenye Ukumbi wa
Mwalimu Nyerere, jijini Dar es Salaam.
Kongamano hilo limeandaliwa na Taasisi hiyo ya (NIMR). Kushoto ni
Mkurugenzi wa NIMR, Dkt. Mwele Malecela (katikati) ni Mwenyekiti wa
Baraza la NIMR, Samwel Masele.
Picha ya pamoja na washiriki wa Kongamano hilo. (FS)
Comments