MAN UTD YAKABWA KOO NA EVERTON, YAPIGWA 2-0, ARSENAL YAITANDIKA 0 – 3 HULL CITY




Wayne Rooney Manchester UnitedHuenda ndoto za kucheza michuano za UEFA mwakani huenda zikafifia kufuatia kikosi cha Mashetani wekundi, timu ya Manchester United kuchezea kipigo cha bao mbili kwa bila na vijana wa zamani wa Moyes Everton katika mchezo uliochezwa kwenye dimba la Goodson Park.
Everton
Mkwaju wa penalti uliopigwa na Leighton Baines wa Everton uliweza kufungua njia magoli kabla ya Kevin Mirallas kupachika bao la pili na kufanya matokeo kuwa  2 – 0 huku timu hiyo ikishikilia nafasi ya 4 ikiwa na pointi 69 mkononi ikiacha hatua 12 United.
Mtanange mwengine uliokuwa wa vuta ni kuvute, ulikuwa ni kati ya vibonde Hull City iliyowakaribisha nyumbani kwao Arsenal na kujikuta wakichezea goli 3 kwa nunge kupitia kwa Aaron Ramsey, Lukas Podolski dk ya 45′ na 54′ na hatimaye mchezo kumalizika kwa Arsenal kuibuka kifua mbele kwa ushindi wa bao tatu kwa bila dhidi ya vijana hao wa KC Stadium.
Arsenal
Kwa upande wa majogoo wa jiji la London, klabu ya  Liverpool iliweza kuendeleza kauli mbiu yao ya kusalia kileleni baada ya kuichakaza Norwich City kwa jumla ya bao 2 -3, zilizoiwesha kuwa kileleni kwa pointi 80 mkononi huku ikiwa imebakisha michezo kadhaa kuweza kunyakua kombe la ligi kuu.
LiverpoolTazama video za magoli hapo chini

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA