Huenda
ndoto za kucheza michuano za UEFA mwakani huenda zikafifia kufuatia
kikosi cha Mashetani wekundi, timu ya Manchester United kuchezea kipigo
cha bao mbili kwa bila na vijana wa zamani wa Moyes Everton katika
mchezo uliochezwa kwenye dimba la Goodson Park.
Mkwaju wa penalti uliopigwa na Leighton Baines wa Everton
uliweza kufungua njia magoli kabla ya Kevin Mirallas kupachika bao la
pili na kufanya matokeo kuwa 2 – 0 huku timu hiyo ikishikilia nafasi ya
4 ikiwa na pointi 69 mkononi ikiacha hatua 12 United.
Mtanange mwengine uliokuwa wa vuta ni kuvute, ulikuwa ni kati
ya vibonde Hull City iliyowakaribisha nyumbani kwao Arsenal na kujikuta
wakichezea goli 3 kwa nunge kupitia kwa Aaron Ramsey, Lukas Podolski dk
ya 45′ na 54′ na hatimaye mchezo kumalizika kwa Arsenal kuibuka kifua
mbele kwa ushindi wa bao tatu kwa bila dhidi ya vijana hao wa KC
Stadium.
Kwa upande wa majogoo wa jiji la London, klabu ya Liverpool
iliweza kuendeleza kauli mbiu yao ya kusalia kileleni baada ya
kuichakaza Norwich City kwa jumla ya bao 2 -3, zilizoiwesha kuwa
kileleni kwa pointi 80 mkononi huku ikiwa imebakisha michezo kadhaa
kuweza kunyakua kombe la ligi kuu.
Comments