MECHI YA SIMBA NA YANGA YA KUFUNGA PAZIA LA LIGI KUU YASHINDWA KUPATA MBABE, ZATOKA SARE YA 1 -1


Simba1
Pazia la ligi kuu Tanzania bara limefungwa rasmi hii leo kwa timu zote 14 kushuka dimbani , huku miamba miwili ya soka Tanzania, Yanga na Simba wakitoka sare ya goli moja moja. 
Simba ndio waliokuwa wa kwanza kupata bao kipindi cha pili cha mchezo, likifungwa kiustadi kabisa na Harun Athuman Chanongo  na baada ya dakika takribani tano mbele, Yanga iliweza kusawazisha kupitia  winga wake wa pembeni  Simon Msuba kupitia pande alilopigiwa na Didier Kavumbagu na mchezo kumaliza kwa sare ya bao moja kwa moja na yanga kuweza kukabidhiwa kombe lake la mshindi wa pili.
Yanga1Hamis Kiiza  wa Yanga na beki wa timu ya Simba Nassor Masoud.
Mbali na mchezo huo, kituko kikubwa kilichotokea leo katika uwanja wa Taifa, ilikuwa ni katika lango la timu ya Simba kulikuwa na taulo ambalo mlinda mlango wa Simba ‘Ivo Mapunda’ alilokuwa anajifutia mara zote wakati anataka kudaka mipira akiwa amelitundika katika nyavu, kitendo kilichotokea kumkera mchezaji mmoja wa Yanga na kulichukua kisha kulirusha upande wa mashabiki na kushangiliwa sana.
Lakini kocha wa Simba ‘Zdravko Logarusic‘ alionekana kutopendezwa na tukio hilo na kuamua  kumpa  mchezaji wa akiba taulo lake akalipeleka tena langoni kwa timu wa Simba kabla ya baadae kuja shabiki wa Yanga na kulichukua kisha kutokomea nalo sehemu isiyojulikana.

IvoTaulo lilipozua kizaa zaa.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI