Na. Mwandishi wetu.
Makampuni
matatu makubwa yaliyo ndani ya MeTL Group hivi majuzi yamefanikiwa
kutwaa tuzo za Rais za Watengenezaji Bidhaa kwa mwaka 2013.
Makampuni
hayo ni: East Coast Oils & Fats Ltd ya Kurasini ambayo hutengeneza
sabuni na mafuta ya kupikia pamoja na bidhaa nyingine.
Afritex
Limited ambayo hutengeneza Khanga, Vitenge na bidhaa zifananazo; na
21st Century Textiles ambayo ni kampuni kubwa na ya kisasa Afrika
Mashariki na kati inayotengeneza bidhaa kama khanga, vitenge, vikoi,
mashuka, nguo za kimasai n.k.
Tuzo
ya Rais ya Watengenezaji wa Bidhaa ni tuzo ambayo hutolewa kwa
makampuni mbali mbali nchini Tanzania yanayojihusisha na utengenezwaji
wa bidhaa. Ubora wa bidhaa ndio hufanya kampuni kushinda tuzo hiyo.
Comments