Msanii
maarufu nchini Tanzania Kutoka kundi la Orijino Komedi al maarufu kama
Mpoki a k a Muarabu wa Dubai anatarajiwa kuondoka nchini mapema mwanzo
wa wiki hii kwenda nchini Ujerumani kuhudhuria Mkutano mkuu wa Umoja wa
Watanzania Ujerumani (U T U), utakaoambatana na Kongamano la kibiashara
pamoja na Sherehe za Muungano wa Tanzania , zitakazoanza siku ya
ijumaa tarehe 25.04.14 na kumalizika siku ya Jumamosi Tarehe 26.04.14.
Mpoki
amesema kuwa umuhimu mkubwa wa safari yake ni kuwakilisha wasanii wa
Tanzania katika Tamasha hili kubwa la aina yake, na kufafanua kuwa
wakati umefika kwa wasanii wa Tanzania kushirikiana kikamilifu na
Watanzania wanaoishi nje ya nchi ili kuweza kupata fursa mbali mbali
zilizopo huko.
Amesema
amevutiwa sana na Umoja Wa Watanzania Ujerumani (U T U) kwa shughuli
zake mbali mbali ambazo umekwishazifanya nchini humo na ameamua kutoa
mchango wake wa hali na mali kuhakikisha (U T U) inafanya vizuri
zaidi na kwamba yeye binafsi amekuwa ni mfuatiliaji wa karibu sana wa
shughuli za umoja huo.
Mwenyekiti
wa Umoja Wa Watanzania Ujerumani Bw. Mfundo Peter Mfundo alithibitisha
safari ya msanii huyo Maarufu nchini Tanzania, na kusema U T U
Ilipendelea sana wasanii zaidi kuhudhuria sherehe hizi lakini kwa bahati
mbaya haikuwezekana kutokana na mambo yalio nje ya uwezo wao ingawa
UTU ni chombo kinachokubali sana na kuzifagilia kazi za wasanii wa
Tanzania.
U T U inamtakia Bw Mpoki Safari njema.
Comments