Hatimaye ratiba imetoka ya timu zitakazomenyana katika hatua ya nusu fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa ya ulaya.
Mabingwa mara tisa wa klabu bingwa ya Ulaya timu ya Real
Madrid itawakaribisha nyumbani wapinzani wao Bayern Munich ‘The
Bavarian’ katika mchezo wa mkondo wa kwanza utakaochezwa April 23 na
kurejeana tena baada ya siku nane baadae.
Nusu fainali ya pili itakuwa kati ya Atletico Madrid
itakialika kikosi cha ‘The Blues’ Chelsea’ kwenye dimba lao la ‘Vicent
Calderon’ April 22 na baada ya siku nane watawafuata darajani Stamford
Bridge.
Comments