Meneja
Mradi wa Asasi ya Kijamii ya The Open Society Initiative For Eastern
African Tanzania (OSIEA), Agnes Hanti akiongea wakati wa mafunzo kwa
wadau wa Habari nchini juu ya changamoto zinazowakabili waandishi wa
habari hasa katika haki ya kukuza demokrasia kwa waandishi wa habari
yaliyofanyika leo Aprili 2, 2014 jijini Dar es Salaam.
Meneja
Mradi wa Asasi ya Kijamii ya The Open Society Initiative For Eastern
African Tanzania (OSIEA), Agnes Hanti akiongea wakati wa mafunzo kwa
wadau wa Habari nchini (hawapo pichani) juu ya changamoto zinazowakabili
waandishi wa habari hasa katika haki ya kukuza demokrasia iliyofanyika
jijini Dar es Salaam. Pembeni ni Mkurugenzi Msaidizi wa OSIEA, Mburu
Gitu (Kulia).
Meneja
Mradi wa Asasi ya Kijamii ya The Open Society Initiative For Eastern
African Tanzania (OSIEA), Agnes Hanti akiongea na waandishi wa habari
wakati wa majadiliano.
Waandishi
wa Habari na wadau wa Habari nchini wakijadili juu ya changamoto
zinazowakabili katika haki ya kukuza demokrasia iliyofanyika jijini Dar
es Salaam.
Mkurugenzi
wa Chuo Cha Uandishi wa Habari za Kibiashara (EABMTI), Bi. Rosemary
Mwakitwange akifafanua changamoto mbali mbali zinazowakabili wanahabari
mara baada ya kumalizika kwa mafunzo hayo.
Waandishi
wa Habari na wadau wa Habari nchini wakijadili juu ya changamoto
zinazowakabili katika haki ya kukuza demokrasia iliyofanyika jijini Dar
es Salaam.
Waandishi
wa Habari na wadau wa Habari nchini wakijadili juu ya changamoto
zinazowakabili katika haki ya kukuza demokrasia iliyofanyika jijini Dar
es Salaam.
---
Asasi
isiyo kuwa ya kiserikali ya OSIEA imesema kazikubwa inahitajika
kufanyika ili kulinda Uhuru wa kujieleza na kujitegemea kwa vyombo vya
habari nchini Tanzania. Wito huo unatokana na kuongezeka kwa vitendo vya
kufungia vyombo vya habari na kuongezeka kwa matukio ya kuwadhuru
waandishi wa habari pamoja na kuingiliwa kwa Uhuru wa wahariri na
wanasiasa na wafanyabiashara.
Mwaka
jana serikali ili yafungia magazeti binafsi ya Mwananchi na Mtanzania
kwa siku 14 na 90 kwa tuhuma za kuchapisha habari zenye uchochezi ambazo
serikali ilidai zinahatarisha usalama wa taifa na zinatishia uvunjifu
wa amani na umoja.Gazeti jingine la Mwanahalisi liliamriwa kufungwa
tangu mwezi Julai2012 na halijafunguliwa mpaka sasa. Sheria ya magazeti
inaipa serikali mamlaka makubwa ya kukandamiza vyombo vya habari. Hatua
zote hizo zinakwenda kinyume na sheria za nchi na haki za binadamu
ambazo Tanzania imeridhia.
Pamoja
ukweli kuwa vyombo vya habari binafsi vinaongezeka tangia mwaka 1990
lakini Uhuru wa wahariri wa vyombo hivyo bado una maswali mengi
kuhusiana na baadhi ya vyombo kutumika kutanga biashara na kuwasaida
wengine kisiasa. OSIEA inaitaka serikali na vyombo vya usalama kuheshimu
Uhuru wa kujieleza na kutoa maoni na kuacha kuwanyanyasa waandishi wa
habari. Waandishi wa habari lazima waweze kuzungumza na kuandika bila ya
kuwepo kwa vizuizi vyovyote. OSIEA pia inaitaka serikali kuwasilisha
Bungeni muswaada wa sheria ya vyombo vya habari ambao utaweka mazingira
bora ya Uhuru wa vyombo vya habari.
Wakati
Tanzania ikiwa katika maandalizi ya kupata katiba mpya, tunahitaji
kukumbuka kuwa Uhuru wa vyombo vya habari na Uhuru wa kujieleza kwa
waandishi wa habari ni kitu cha muhimu kwa ajili ya kusambaza taarifa
kwa jamii. Sio tu haki ya jamii kupokea taarifa bali bila kuwa na Uhuru
haitakuwa na maana yoyote kwa serikali yao. Uwezo wa kupata taarifa
utawezesha kukua kwa demokrasia, kuongeza msisismko wa mijadala ya
kitaifa kutoa taarifa zitakazoongeza uwajibikaji. Uhuru wa kupata habari
una mchango mkubwa katika mchakato wa kupata Katiba mpya.
Licha
ya kwamba Tanzania inakuza uchumi wake wa wakati lakini kusahau Uhuru wa
vyombo vya habari kunaweza kukapunguza ufanisi wa ukuaji wa uchumi.
Vyombo vya habari huru vinaweza kukuza kuimarisha jamii na kuvutia
wawekezaji.
Comments