Mwanamuziki wa Bongo fleva ‘Shetta’ ei kei ei baba Qayllah
amenusurika ajali mbaya alipokuwa njiani akielekea Babati mkoani
Manyara kwa ajili ya ziara yake ya muziki ‘Kerewa Tour’ iliyokuwa
ifanyike jana usiku.
Arusha
1#babati leo ndo siku yenu ile #kerewatour ofcoz mi ndo baba Qayllah…
sikiliza mi sirudi nyuma alafu kushoto na kulia hakuna deal kama vipi we
#angaliambeleeee. Picha na ujumbe Alioandika
Shetta kupitia ukurasa wake wa Instagram baada ya kutua kwenye uwanja
wa ndege wa Arusha akitokea Dar kabla ya ajali kutokea.
Kwa mujibu wa taarifa zinasema kwamba, staa huyo wa
‘Nidanganye’ alipofika jijini Arusha akitokea Dar, alipokelewa na
wenyeji wake na kisha safari kuanza kuelekea Babati.
Ripoti iliongeza kuwa, walipofika eneo moja lenye mbuga,
ghafla alikatisha pundamilia hali iliyopelekea gari alilopanda msanii
huyo kupinduka mara tatu kutokana na dereva wa gari hilo kufunga breki
kwa minajili ya kumkwepa mnyama huyo.
Picha ni gari aina ya Toyota Noah alilokuwemo Shetta baada ya kuanguka mara tatu.
”nashukuru mungu nimetoka salama kweli mungu mkubwa mana
nilijua leo ndo mwisho wangu mana ajali ni mbayaaa sanaaaaa…… thnx
woteee mlionipa pole tupo pa1” aliandika Shetta.
Blogu ya Larrybway91 inampa pole mwanamuziki Shetta na kumtakia afya njema.
Comments