Ikulu
ya Whitehouse imeikashifu kampuni ya simu ya Samsung kwa kutumia picha
ya Rais Barack Obama aliyojipiga na mchezaji maarufu nchini Marekani
David Ortiz kama tangazo la kibiashara.
Picha hiyo ilipigwa na Ortiz mwenyewe akiwa na Rais Obama akitumia simu yake ya Samsung mapema wiki.
Hata
hivyo kampuni ya Samsung iliisambaza kupitia kwa mtandao wa kijami wa
Twitter kwa wateja wake na watu milioni 5.2 wanaoifuata kwa Twitter.
Msemaji
wa Ikulu ya White House, Jay Carney, alisema kuwa picha ya Rais
haipaswi kwa njia yoyote kutumiwa kwa sababu za kujinufaisha kibiashara.
Wakuu wa Samsung hawajasema lolote kuhusu malalamiko ya White House.
Bwana Carney amesema kuwa mawakili wa White House wanashauriwa kuhusu kitendo hicho cha Samsung.
"bila ya kusema mambo mengi, nataka niwaambie tu kwamba White House inapinga vikali jambo hili,'' alisema Carney
Ortiz
alimpa Rais Obama Jezzi maalum kutoka kwa klabu anayochezea ya Red Sox
ikiwa na jina la Rais siku ya Jumanne na jkisha kumshawishi kujipiga
naye picha mwenyewe inayojulikana kama 'Selfie'.
"Nilimpa Jezzi na wapiga picha waka wanatupiga picha, basi nilijhisi na mimi kujipiga naye picha'' alisema mchezaji huyo.
Alikana kuwa kampuni ya Samsung ilimlipa pesa kwa picha hio.Chanzo BBC Swahili
Comments