Pistorius aanza kujitetea mahakamani



Oscar Pistorius akilia alipokuwa chumba cha mahakama Februari 2013
Oscar Pistorius akiwa amejaa majonzi ameanza kutoa utetezi wake katika kesi ya mauaji inayomkabili kwa kuwaomba radhi familia ya rafiki yake wa kike aliyeuawa Reeva Steenkamp.
Kwa sauti ya kutetema, amesema alikuwa "akijaribu kumlinda" na amesema anashindwa kujua uchungu wanaoupata.
Bwana Pistorius amesema anasumbuliwa na"ndoto za kutisha" na mara nyingi aliamka na kusikia harufu ya damu ya Bi Steenkamp.
Waendesha mashitaka wanasema Pistorius alimuua Steenkamp mwezi Februari 2013 baada ya kuzozana. Pistorius anasema alidhani ni jambazi.
Mwanaridha huyo mwenye ulemavu wa miguu amewaambia ndugu wa Bi Steenkamp kwamba "hakuna wakati ambao ameshindwa kufikiria juu yao tangu mkasa huu utokee".
"Naamka kila siku asubuhi na ninyi ni watu wa kwanza kuwafikiria, watu wa kwanza ninaowaombea. Sifahamu uchungu na mawazo na ukiwa ambao nimewasababishia ninyi na familia yenu.
" Nilikuwa najaribu kumlinda Reeva. Nawahakikishia kuwa alipokwenda kulala usiku ule alihisi kupendwa".
"nimejaribu kuandika maneno yangu mengi kwenye karatasi. Mara nyingi kuwaandikia. Lakini hakuna maneno yatakayotosheleza maelezo yangu."
Amesema anatumia dawa za kuzuia msongo wa akili na kukosa usingizi.
"Naogopa kulala, Nimekuwa na ndoto za kutisha, Nasikia harufu ya damu na kuamka nikiwa mwoga.," amesema.
Amesema kamwe hataki kumiliki silaha.Chanzo BBC Swahili

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI