Oscar
Pistorius akiwa amejaa majonzi ameanza kutoa utetezi wake katika kesi ya
mauaji inayomkabili kwa kuwaomba radhi familia ya rafiki yake wa kike
aliyeuawa Reeva Steenkamp.
Kwa sauti ya kutetema, amesema alikuwa "akijaribu kumlinda" na amesema anashindwa kujua uchungu wanaoupata.
Bwana Pistorius amesema anasumbuliwa na"ndoto za kutisha" na mara nyingi aliamka na kusikia harufu ya damu ya Bi Steenkamp.
Waendesha
mashitaka wanasema Pistorius alimuua Steenkamp mwezi Februari 2013
baada ya kuzozana. Pistorius anasema alidhani ni jambazi.
Mwanaridha
huyo mwenye ulemavu wa miguu amewaambia ndugu wa Bi Steenkamp kwamba
"hakuna wakati ambao ameshindwa kufikiria juu yao tangu mkasa huu
utokee".
"Naamka
kila siku asubuhi na ninyi ni watu wa kwanza kuwafikiria, watu wa
kwanza ninaowaombea. Sifahamu uchungu na mawazo na ukiwa ambao
nimewasababishia ninyi na familia yenu.
" Nilikuwa najaribu kumlinda Reeva. Nawahakikishia kuwa alipokwenda kulala usiku ule alihisi kupendwa".
"nimejaribu
kuandika maneno yangu mengi kwenye karatasi. Mara nyingi kuwaandikia.
Lakini hakuna maneno yatakayotosheleza maelezo yangu."
Amesema anatumia dawa za kuzuia msongo wa akili na kukosa usingizi.
"Naogopa kulala, Nimekuwa na ndoto za kutisha, Nasikia harufu ya damu na kuamka nikiwa mwoga.," amesema.
Amesema kamwe hataki kumiliki silaha.Chanzo BBC Swahili
Comments