Na Andrew Chale
WAPENZI
wa nyimbo za zamani za taarabu asilia nchini, jumapili hii ya Aprili
20, ya Pasaka.. wanatarajiwa kupata burudani safi na zawadi nyingi
zitakazotolewa na Fabak Fashion ndani ya ukumbi wa Regency Hotel,
Mikocheni, jijini Dar es Salaam.
Kwa
mujibu wa Mkurugenzi wa Fabak Fashions, Asia Idarous Khamsin, miongoni
mwa wadhamini wa onesho hilo, amewaomba wadau kujitokeza kwa wingi
kufurahia usiku huo kwa kukumbushiana enzi sambamba na zawadi lukuki
zitakazotolewa kwa njia ya bahati nasibu.
Asia
Idarous alisema onesho hilo la kila Jumapili, usiku huo wa ‘Old is
Gold na Spice Modern Taarab,’ pia watafurahia pamoja na wadau katika
kusherehekea Pasaka, ambapo wasanii nguli waalikwa watakuwamo.
“Jumapili
hii ndani ya Old is Gold, pia wasanii Mwanahawa Ally na Rukia Ramadhan,
watakuwapo kuwasindikiza Spice Modern taarab, hivyo shamrashamra kuwa
kubwa zaidi,” alisema Asia Idarous.
Kuhusu
kiingilio, alisema kitakuwa sh 5,000 tu, watafurahia burudani hiyo ya
aina yake zikiwemo nyimbo za mwambao hasa zile zilizokuwa zikipendwa,
kuanzia saa 12 jioni hadi saa sita usiku sambamba na kuchezesha bahati
nasibu na kugawa zawadi kutoka Fabak Fashion.
Asia
Idarous alizitaja baadhi ya nyimbo wanazotamba nazo wasanii hao
waalikwa ni ‘Nikumbatie’ wa Rukia Ramadhan na ‘Usiku wa Awali’ wa
Mwanahawa Ally.
Wadhamini wengine katika usiku huo wa taarabu asilia ni Times FM, Regency Park Hotel na Fabak Fashions.
Comments