Salamu za Pasaka 2014 toka Chama Cha Mapinduzi Uingereza.


Chama  Cha Mapinduzi- London – Uingereza  kinaridhia Salaam za CCM Makao Makuu kuungana na Wakristo- Watanzania na Ulimwenguni kote  kuwatakia kila la kheri na fanaka katika kusherehekea Sikuu Kuu ya PASAKA 2014.

Aidha CCM UK  inayo imani kubwa kuwa Sherehe hii ya Pasaka itakuwa kigezo cha kuwakaribisha Watanzania wa Imani zote kujitazama kwa wongufu na kuridhia misingi mikuu ya Uhuru, Muungano wetu na Umoja wa Taifa letu.

CCM UK inaungana na Watanzania wote kukememea dhidi ya vichocheo vya aina zote vinavyohatarisha umoja wa TAIFA LETU, usalama wa raia na mali zao, uhuru wao wa kuabudu na kusujudu ndani na nje ya mipaka ya Tanzania.

Kwa kuwa Dhamira kuu ya Pasaka ni kujenga Upendo, Mshikamano, Umoja na Uhuru, hasa katika kipindi hiki cha kutafakari mchakato wa Kupata KATIBA MPYA yenye kukidhi kiu ya maendeleo kwa Wananchi Kiuchumi na kimaendeleo kama Taifa moja, CCM UK inawatakia kila la kheri katika kusheherekea sikukuu hii muhimu kwa Wakristo wote Duniani kwa Amani na Utulivu.

MUNGU IBARIKI TANZANIA.

Imetolewa na Abraham Sangiwa -  Idara ya Siasa na Uenezi.
CCM –  TAWI LA UINGEREZA - UNITED KINGDOM.
20th April -2014

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

𝙂𝘼𝙈𝙊𝙉𝘿𝙄 𝙆𝘼𝘾𝙃𝙀𝙕𝘼 𝙆𝙄𝘽𝙄𝙉𝙂𝙒𝘼.