Serikali yapania Kuondoa Tatizo la Dawa katika Hosipitali za Umma

 Mkurugenzi wa shughuli za Kanda na Huduma kwa wateja  toka Bohari ya Dawa (MSD) Bw. Edward Terry Kulia akizungumza na waandishi wa habari  leo katika ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo  juu ya mpango wa bohari hiyo kupanua maghala  ya kuhifadhi Dawa na Vifaa  tiba kama moja ya hatua za kuboresha huduma zinazotolewa na Bohari hiyo . Kushoto ni Mkurugenzi  wa Manunuzi wa Bohari hiyo  Bw. Heri Mchunga.
Mkurugenzi  wa Manunuzi  Bohari ya Dawa (MSD) Bw. Heri Mchunga akielezea kwa waandishi wa habari  jinsi Serikali inavyodhibiti wizi wa Dawa kwa kuweka nembo maalumu ambapo hadi sasa tayari dawa 20 zimewekewa nembo hiyo. Kulia ni Mkurugenzi wa shughuli za Kanda na Huduma kwa wateja  Bohari ya Dawa Bw. Edward Terry.

=======  ======
Na Frank Mvungi-Maelezo
Serikali yajipanga kuhakikisha upatikanaji wa dawa unakuwa wa uhakikika katika hosipitali zote za umma hapa nchini.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa shughuli za Kanda na Huduma kwa wateja wa Bohari ya dawa (MSD) Bw.Edward Terry  wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam.
Akieleza Terry amesema kwa hivi sasa Bohari ya Dawa imejipanga vizuri kuhakikisha kuwa dawa zinafika kwa wakati katika  maeneo yote zinakohitajika  kwa kuweka mfumo mzuri unahakikisha kuwa  dawa zikifika  zinatumika kwa wananchi waliokusudiwa .
Akieleza Zaidi Terry alisema kuwa mnamo mwaka 2010 walifanya majaribio ya utaratibu wa kupeleka dawa moja kwa moja kwenye vituo vya afya ambapo utaratibu huu umeonyesha mafanikio makubwa hivyo ni imani ya Bohari ya Dawa kuwa utaratibu huo utasaidia sana kuondoa tatizo la upatikanaji wa dawa hasa maeneo ya vijijini.
 Kwa upande wa Kudhibiti upotevu wa dawa katika vituo vya Afya na Hosipitali Terry amesema dawa zinazotolewa na Serikali zitakuwa na alama maalum ya kuzitofautisha na zile zinazouzwa katika maduka binafsi ili kuondoa tatizo la wizi wa dawa zinazosambazwa na Bohari ya Dawa hapa nchini.
 Kuhusu Faida za  kuweka alama maalum katika dawa za Serikali Terry amesema utasaidia kwa kiasi kikubwa kuondoa  malalamiko ya wananchi kuhusu upatikanaji wa dawa mara wanapahitaji huduma hiyo katika hosipitali au vituo vya afya kwa kuwa tatizo la wizi  litakoma.
Kwa wale watakaobainika kujihusisha na wizi wa dawa za Serikali  ,Terry amesema hatua kali zitachukuliwa  bila kuwaonea haya na kutoa wito kwa wananchi kuwafichua wale wote wanaojihusisha na wizo huo ili mkondo wa sheria uchukue nafasi yake.
Bohari kuu ya Dawa imefungua kituo cha Kusambaza Dawa cha Muleba ,Mkoani  Kagera kitakachosaidia kuwahudumia wananchi wa Mkoa wa Geita na Kagera kwa kuwasogezea huduma hiyo karibu.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA