SOMA TAARIFA KWA UMMA KUTOKA HIFADHI ZA TAIFA TANZANIA(TANAPA):WATALII MABILIONEA WA MAREKANI WAMALIZA ZIARA SERENGETI
Watalii
Mabilionea 42 kutoka Marekani wamemaliza ziara yao ya utalii ya siku
nne katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na kuelezea kufurahishwa kwao
na uzuri wa hifadhi pamoja na maajabu ya wanyama mbalimbali
wanaopatikana Serengeti ikiwemo msafara maarufu wa wanyama wahamao aina
ya nyumbu.
Waziri
wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu alipata fursa ya kuwaaga watalii
hao walipokuwa wakiondoka nchini kuendelea na ziara ya utalii katika
nchi nyingine za Afrika wakitumia ndege binafsi aina ya Boeing BBJ 737
HB-11Q inayomilikiwa na Kampuni ya Utalii ya Abercrombie & Kent ya
nchini Marekani.
Comments