Habarini
Bloggers, Napenda kuchukua nafasi hii kuwapa taarifa kuwa Blog ya
Kijiwe Cha Wasomi iliyokuwa na makazi yake Wilayani Bahi katika mkoa wa
Dodoma, sasa itahamia Mtwara mjini.
(Gas City). Hii ni kutokana na majukumu mengine ya kitaifa yanayofanywa
na mwongozaji wa blog hii. Bado hatujajua ni eneo gani tutaweka ofisi
zetu mkoani Mtwara, lakini nitawataarifu mara baada ya kukamilisha
taratibu zote.
Pamoja na mabadiliko haya, utendaji wa blog hauta athiriwa.
Karibuni sana Gas City.
Elly Marimbocho,
Admin Kijiwe Cha Wasomi
Comments