Toyota yaregesha magari milioni 6

Toyota yaagiza magari milioni 6.5 
kurejeshwa viwandani
Kampuni kubwa ya uundaji na uuzaji wa magari ya Japan, Toyota i meagiza magari milioni sita unusu kurejeshwa ilikufanyiwa ukarabati kutokana na upungufu mbalimbali.
Idadi hiyo ya kurejeshwa magari ni kubwa mno kurejeshwa viwandani.
Kampuni hiyo kubwa zaidi duniani ya uundaji magari inarejesha magari aina ya Yaris, Urban Cruiser, RAV4 na Hilux.
Kuna hitilafu katika kifuko cha hewa cha kumlinda dereva -(air bag) katika jumla ya magari milioni tatu, ikiwa haiwezi kuchomoka ili kimlinda dereva wakati wa ajali.
Aidha kuna hitilafu pia katika baadhi ya viti, usukani na kifaa cha mota ya kuwasha magari.
Kampuni ya Toyota inasema haijabaini ni ajali ngapi, majeruhi au maafa ambayo yamesababishwa na matatizo hayo yaliyogundulika majuzi.
Jumla ya magari 20,000 yanahitilafu ya mota ya kuwasha.
Mwezi Februari, Toyota iliagiza magari milioni 1.9 aina ya Prius hybrid yaregeshwe kutokana na hitlafu iliyopelekea magari hayo kupoteza mwendo ghafla.

Kwa Jumla magari milioni 25 yamearegeshwa katika kipindi cha miaka miwili u nusu iliyopita.Chanzo BBC Swahili

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI