Viingilio Tamasha la Pasaka hadharani,kufanyika uwanja wa Taifa

 Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi, Alex Msama akizungumza na baadhi ya Wanahabari kwenye moja ya mikutano yake kuhusiana na tamasha la pasaka.
KAMATI ya Maandalizi ya Tamasha la Pasaka, mwishoni mwa wiki ilitangaza viingilio vya tamasha hilo jijini Dar es Salaam, viti vya kawaida ni shilingi 5000 na watoto 2000. Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi, Alex Msama viti maalum ni shilingi 20,000 wakati VIP  ni shilingi 10,000.
 Msama alisema hivi sasa wanaendelea na mchakato wa kufanikisha zoezi la mgeni rasmi katika tamasha hilo kwani hivi karibuni watakamilisha zoezi la upigaji kura kumchagua.
Msama alisema mchakato wa kuelekea katika tamasha hilo litakalofanyika jijini Dar es Salaam Aprili 20 na baadaye mikoa mingine saba hapa nchini.
 Aidha Msama alitoa wito kwa wakazi wa Dar es Salaam kujiandaa na tamasha hilo ipasavyo kwani lina mlengo wa kurudisha mapato yanayopatikana na kuyapeleka katika maeneo matatu ambayo yanawahusu, yatima, walemavu na wajane.

 Msama alisema mipangilio yake ya kuwawezesha wenye uhitaji maalum ni kuwajengea kituo kitakachokuwa katika eneo la Pugu nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam ambacho kitajulikana kama Jakaya Mrisho Kikwete, rafiki wa wasiojiweza.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*