VIJANA WA NYEGEZI MWANZA WAHAMASISHWA KUJITOKEZA KWA WINGI KATIKA SHINDANO LA KUSAKA VIPAJI VYA UIGIZAJI

 Msanii wa Filamu Tanzania Elizabeth Michael (Lulu) akikumbatiana na Mmoja wa Mashabiki wa Filamu zake katika Eneo la Nyegezi Mwanza Jioni ya Leo wakati wasanii wa filamu Tanzania walipotembelea eneo hilo kwa lengo la kutambulisha Shindano la Kusaka Vipaji vya Uigizaji Tanzania lijulikanalo kama Tanzania Movie Talents litakaloanza kesho Mkoani Mwanza, Mahali ni Isamilo Lodge
Baadhi ya Wakazi wa Nyegezi Mwanza wakiwa wamekusanyika kwaajili ya kuwashuhudia wasanii wa filamu Tanzania waliofika katika Viwanja hivyo vya Stendi ya Nyegezi kwaajili ya Kutambulisha Shindano la Kusaka Vipaji vya Kuigiza Tanzania litakaloanzia Jijini Mwanza.
 Kijana Mmoja wa Kike ambaye jina lake halikuweza kupatikana haraka akionyesha jinsi ya kushtua Kijoti joti wakati wasanii wa filamu Tanzania Walipofika katika Viwanja vya Stendi ya Nyegezi jioni ya leo
 Msanii wa Vichekesho Joti akimchagua mmoja wa wakazi wa Nyegezi Mwanza kwaajili ya Kupewa zawadi kutoka kwake
 Lulu akiongea na wakazi wa Nyegezi Mwanza wakati walipotembelea Viwanja vya Stendi ya Nyegezi jioni ya Leo
 Baadhi ya wakazi wa Nyegezi wakinyoosha vidole kwaajili ya kuchaguliwa kujibu swali ambapo mshindi alijishindia Zawadi ya Kopi moja wapo ya Filamu ya Msanii Lulu
 Lulu akimkabidhi Zawadi ya Filamu yake ya Foolish Age kijana ambae alipatia kumtaja jina lake halisi wakati wasanii hao walipotembelea viwanja vya Nyegezi Mwanza 
 Picha ya Pamoja na Mshindi wa zawadi ya Filamu
 Msanii Rich Rich akiongea na wakazi wa Nyegezi Jioni ya Leo
 Msanii wa Filamu Tanzania Steve Nyerere ambe pia ni Mwenyekiti wa Bongo Movie akiongea na wakazi wa Nyegezi Jioni ya leo wakati wasanii walipotembelea viwanja vya stendi ya nyegezi kwaajili ya Kutambulisha na kuwahamasisha vijana na wazee kujitokeza kwa wingi kwaajili ya kuonyesha Vipaji vyao Vya kuigiza katika Shindano la Kuigiza lijulikanalo kama Tanzania Movie Talents ambalo linaanza rasmi Kesho jijini Mwanza mahali ni Isamilo Lodge
Wakazi wa Nyegezi Mwanza wakichungulia kwenye gari walilopanda wasanii wa kuigiza Tanzania ambao walifika katika Viwanja vya Stendi ya Nyegezi kwaajili ya kuhamasisha vijana kwa wazee kuweza kujitokeza kwa wingi Hapo Kesho katika Shindano la Kusaka Vipaji vya Kuigiza Tanzania lijulikanalo kama Tanzania Movie Talents ambalo litafanyika Isamilo Lodge kuanzia Saa Moja asubuhi na Hakuna Kiingilio.Picha na Josephat Lukaza wa Lukaza Blog

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.