Naibu Waziri wa
Nishati na Madini anayeshughulikia nishati, Mhe. Charles Kitwanga katikati
akisisitiza jambo wakati wa kikao na Mameneja wa Tanesco wa wilaya katika Mikoa
ya Mtwara na Lindi (hawapo pichani). Pamoja nae ni watendaji wakuu wa Tanesco Mikoa
ya Lindi na Mtwara. Kikao hicho kilijadili maendeleo ya utekelezaji wa mradi wa
kuunganisha umeme vijijini kupitia REA na namna ya kuvifikia vijiji ambavyo
havijafikiwa katika utekelezaji wa mradi huo awamu ya pili.
Baadhi ya Mameneja
wa Tanesco wa Wilaya katika Mikoa ya Lindi na Mtwara wakimsikiliza Naibu Waziri
wa Nishati nayeshughulikia Nishati Mhe. Charles Kitwanga (hayupo pichani) wakati wa kikao. Mhe.
Kitwanga alisisitiza ubunifu na kuhakikisha mameneja hao wanapunguza tatizo la
kukatikakatika kwa umeme katika Mikoa hiyo.
Kaimu Meneja wa
Kituo cha kuzalisha umeme cha Tanesco- Mtwara
Mhandisi Didas Maleko ( wa pili kulia) akimwongoza Naibu Waziri wa
Nishati na Madini (Nishati) Mhe. Charles Kitwanga kuangalia mitambo
inayozalisha umeme katika kituo hicho. Kwa mujibu wa maelezo ya Maleko, kituo
hicho kina uwezo wa kuzalisha kiasi cha megawati 18.
Mhe. Naibu Waziri
akitoka kuangalia maendeleo ya ujenzi wa bomba katika eneo la Somanga. Nyuma
linaloonekana ni sehemu ya bomba la gesi la nchi 36 ambalo linaelekea Dar es Salaam katika eneo la Kinyerezi
likitokea Mtwara.
Msimamizi
wa Kituo cha kuzalisha umeme wa gesi asilia cha Somanga Mhandisi .
======== ======= ======
Wananchi Changamkieni Mradi wa REA – Kitwanga
Na Asteria Muhozya, Mtwara
Naibu Waziri wa
Nishati na Madini anayeshughulikia Nishati Mhe. Charles Kitwanga, amewataka wananchi
waliopo katika vijiji vinavyopitiwa na Mradi wa kuunganisha Umeme Vijijini
unaosimamiwa na Wakala wa Umeme vijijini (REA) kuchangamkia fursa hiyo wakati
ambao mradi huo unatekelezwa kwa kuwa gharama zake ni nafuu.
Mhe. Kitwanga aliyasema
hayo jana wakati wa kikao chake na Mameneja wa Shirika la Umeme Tanzania
(TANESCO) wa Wilaya za Lindi na Mtwara
waliokutana kwa lengo la kujadili maendeleo ya mradi wa kuunganisha
umeme Vijijini katika Wilaya za mikoa
hiyo unaosimamiwa na REA, ikiwa ni pamoja na kuweka mikakati ya pamoja ya namna
ya kuvifikia vijijii ambavyo bado havijafikiwa na mradi huo awamu ya pili.
Aliongeza kuwa,
wananchi walioko katika maeneo ya vijiji ambapo mradi wa REA awamu ya pili unatekelezwa,
wanapaswa kuitumia fursa hiyo vizuri kwa kuwa gharama kubwa za kuunganisha
umeme zimebebwa na serikali kwa kipindi hicho na endapo mradi huo
utakapokamilika watatakiwa kulipa gaharama zote kama kawaida.
Aidha, alizitaja
gharama hizo kwa kipindi cha utekelezaji
wa mradi wa REA awamu ya pili kuwa ni
kiasi cha shilingi 27,000/- ikiwa ni gharama ya kuunganishwa ambayo ni
VAT na gharama za fomu kiasi cha shilingi 5000/-
Katika hatua
nyingine Mhe. Kitwanga aliwataka Mameneja wa Tanesco kuhakikisha wanapunguza
tatizo la kukatikakatika kwa umeme katika Mikoa ya Lindi na Mtwara na kuhakikisha wanaweka mipango endelevu ya
upatikanaji wa nishati hiyo kutokana na kwamba mikoa hiyo inatarajia kuwa na
uwekezaji mkubwa vikiwemo viwanda vya sementi.
Aidha, aliwataka
watendaji hao kuwa wabunifu na kuongeza kasi ya utendaji katika shughuli zao
ili kurejesha imani ya wananchi kuhusu shirika hilo kwa kuzingatia kwamba,
nishati hasa umeme ina mchango mkubwa katika shughuli zote za kiuchumi na
maendeleo ya taifa.
“ Lazima
tuibadilishe Tanesco. Wananchi wanatakiwa waishangae tanesco kwa huduma nzuri
na si vinginevyo. Sitaki umeme ukatike hovyo hovyo. Vaeni viatu mlivyopewa
.Taswira ya tanesco lazima ibadilike”. Aliongeza Kitwanga.
Halikadhalika,
aliwataka mameneja hao kuhakikisha wanakusanya madeni kutoka kwa wadaiwa wote zikiwemo
taasisi za serikali na watu binafsi ili kuwezesha shirika hilo kujiendesha na
kuendelea kutoa huduma kwa wananachi. Hivyo, amewataka wateja wote wanaodaiwa
na shirika hilo kuhakikisha wanalipa
madeni yao ili shirika hilo liendee kutoa huduma stahiki.
Wakati huo huo,
Meneja Mwandamizi wa Kanda ya Dar es
Salaam na Pwani, Mhandisi Mahenge Mugaya alieleza kuwa, tatizo la kukatikakatika
kwa umeme katika mikoa hiyo linaweza kuzuilika na kuongeza kuwa, tayari zoezi la kubadilisha nguzo mbovu limeanza na
kuwekwa mpya. Vilevile, aliongeza kuwa, katika kukamilisha zoezi hilo, tayari
watumishi zaidi wameongezwa kutoka Dar es Salaam kwa ajili ya shughulli ya
kubadilisha nguzo hizo.
Kwa upande wake
Kaimu Meneja wa Kituo cha Tanesco- Mtwara cha kuzalisha umeme katika mikoa ya
Lindi na Mtwara , Mhandisi Didas Maleko, wakati akitoa taarifa ya uzalishaji umeme katika kituo hicho alieleza kuwa, kituo
hicho kinazalisha kiasi cha megawati 18
kutoka katika mashine tisa ambapo kila machine inazalisha kiasi cha megawati 2.
.
Comments