Vikosi
vya serikali Somalia vimefanikiwa kuidhibiti upya ikulu ya rais katika
mji mkuu Mogadishu baada ya wapiganaji wa Al Shabaab kuishambulia.
Maafisa wanasema washambuliaji wapatao watano kutoka kundi la al-Shabab - waliuawa walipoingia katika eneo la ikulu hiyo.
Washambuliaji hao wanadaiwa kulipua bomu lililotegwa kwenye gari karibu na langu kuu la Ikulu hiyo.
Waziri
wa habari na mawasiliano wa Somalia Mustaf Dhuhulow ameambia BBC kuwa
tayari mmoja wa washambuliaji hao amekamatwa na anahojiwa na polisi.
Waziri Mustaf amesema, '' Walishambulia ikulu ya rais saa za jioni. Alikuwa watu washambuliaji watatu pamoja na dereva wao.
Washambuliaji hao waliuawa lakini dereva wao alipata majeraha madogo na anazuiliwa na polisi na kuhojiwa.
Walijaribu
kuvamia Villa Somalia lakini wakakomeshwa. Tutawapa maelezo zaidi
baadaye. Na tutaweza kutoa maelezo zaidi kwa raia wa Somalia na dunia
nzima.''
Hii ni
mara ya pili kwa Al Shabaab kuvamia ikulu ya rais mjini Mogadishu mwaka
huu japo mara ya kwanza walifanikiwa kuingia ndani.
Rais Hassan Sheikh Mohamoud hakuwepo wakati wa shambulio hilo.
Kundi
la wapiganaji wa kiislamu Al shabaab limefukuzwa kutoka mjini Mogadishu
tangu mwaka wa 2011 lakini limekuwa likifanya mashambulio ya kuvizia
tangu wakati huo.
Wanamgambo
hao wanaaminiwa kufanya mashambulio kadhaa pia katika nchi jirani ya
Somalia kama vile Kenya, Uganda na Tanzania kama njia ya kulipiza kisasi
kwa kuingia majeshi ya Umoja wa Afrika nchini Somalia.Chanzo BBC
Swahili
Comments