Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif
Sharif Hamad, akiwasili katika kijiji cha Donge Muwanda kufutari na wananchi wa
kijiji hicho.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif
Sharif Hamad, akijumuika na wananchi wa kijiji cha Donge Muwanda katika futari
ya pamoja.
Mzee Abdulhakim Muhsin Abeid wa kijiji cha Donge
Muwanda, akizungumza kwa niaba ya wananchi wa kijiji hicho baada ya
kufutari pamoja Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif
Hamad.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif
Sharif Hamad, akiitikia dua baada ya kumjuilia hali mzee Foum Denge (kushoto) wa
kijiji cha Matemwe, Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif
Sharif Hamad, akiwafariji baadhi ya wananchi katika ziara yake ya kutembelea
wagonjwa na wafiwa Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Makamu wa Kwanza wa
Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, akiagana na wazee mbali mbali
katika kijiji cha Bumbwini, baada ya kumaliza ziara yake ya kutembelea wagonjwa
na wafiwa katika Mkoa wa Kaskazini Unguja. (Picha zote na Salmin Said,
OMKR)
Na
Hassan Hamad OMKR
MAKAMU
wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad amejumuika pamoja na
wananchi wa kijiji cha Donge Muwanda katika futari ya pamoja aliyoiandaa kwa
ajili ya wananchi wa kijiji hicho.
Akitoa
nasaha zake baada ya futari hiyo, Maalim Seif amewahimiza wananchi wa Donge
kuendeleza umoja na mshikamano walionao, na kamwe wasikubali kugawanywa kwa
sababu zozote zikiwemo za itikadi za kisiasa.
Maalim
Seif ambaye baada ya futari hiyo aliungana na waumini wa kijiji cha Donge katika
sala ya Isha na Tarawehe, amewasisitiza wananchi hao kuendeleza utamaduni wa
kufutari pamoja ambao uliasisiwa tokea wakati wa enzi za Mitume, na kwamba
kufanya hivyo kutakuza mshikamano na mapenzi miongoni
mwao.
Amewashukuru
wananchi hao wa Donge Muwanda kwa kukubali kuungana nae katika futari hiyo,
kitendo ambacho amesema kimempa faraja na matumaini ya kuendelea kwa mshikamano
uliopo nchini.
Mapema
akizungumza kwa niaba ya wananchi wa Donge Muwanda, Mzee Abdulhakim Muhsin
Abeid, amempongeza Maalim Seif kwa uamuzi wake wa kufutari na wananchi wa kijiji
hicho.
Amesema
kitendo hicho kimewaleta pamoja wananchi mbali mbali wa kijiji hicho, na kuomba
utamaduni huo uendelezwe ili kukuza mshikamano na maelewano miongoni mwa
wananchi.
Akizungumzia
kuhusu historia ya kijiji hicho cha Muwanda, Mzee Abdulhakim amesema kijiji
hicho kina historia ndefu tokea wakati wa ukoloni na harakati za kupigania
uhuru.
Wakati huo huo Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar amefanya ziara
ya kuwatembelea na kuwafariji wagonjwa na wafiwa katika vijiji mbali mbali vya
Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Katika
ziara hiyo Maalim Seif amewatembelea wagonjwa na kuwafariji wafiwa katika vijiji
vya Matemwe, Donge, Kitope na Bumbwini, ambapo anatarajiwa kuendelea na ziara
hiyo kwa Mikoa yote ya Unguja na Pemba, ndani ya kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu
wa Ramadhani.
Comments