NAIBU WAZIRI WA WIZARA YA UCHUKUZI DK. CHARLES TIZEBA ATEMBELEA CHUO CHA BAHARI DAR ES SALAAM (DMI) MWANZONI MWA WIKI

                

DSC_0703
Naibu Waziri wa Wizara ya Uchukuzi, Dk. Charles Tizeba akisaini kitabu cha wageni katika ofisi ya Mkuu wa Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI), mara baaada ya kuwasili chuoni hapo kuangalia shughuli mbalimbali zinazofanywa na chuo hicho na kuongea na wafanyakazi wa Chuo hicho, mwanzoni mwa wiki. Kulia kwake anaemtazama ni Kaimu Mkuu wa Chuo hicho, Kapteni Yasin Songoro.
DSC_0712
Mkufunzi wa Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI), akimpa maelezo ya namna ambavyo wahandisi wanaofanya kazi ndani ya chumba cha injini ndani ya Meli wanavyoendesha mitambo hiyo kwa Naibu Waziri wa Wizara ya Uchukuzi, Dk. Charles Tizeba, wakati alipotembea chuoni hapo mwanzoni mwa wiki kuongea na wafanyakazi wa chuo hicho.
DSC_0719
Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dk. Charles Tizeba, akimsikilza Kapteni Jumanne Karume, alipokuwa akimpa maelezo ya namna nahodha anavyoendesha Meli, wakati alipotembelea Chuo Cha Bahari Dar es Salaam(DMI), mwanzoni mwa wiki. Kushoto kwa Dk Tizeba ni Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Kapteni Yasin Songoro.
DSC_0721
Naibu Waziri wa Wizara ya Uchukuzi, Dk. Charles Tizeba (aliyeweka mikono mfukoni), akimsikiliza Kapteni Peter Mkunja wakati akimpa maelezo ya namna vyombo vya kujiokoa vinavyotumika endapo meli itazama ama kupata hitilafu yoyote, wakati Naibu Waziri huyo alipotembelea Chuo hicho Mwanzoni mwa wiki.
DSC_0722
Kaimu Mkuu wa Chuo Cha Bahari Dar es Salaam (DMI), Kapteni Yasin Songoro, akitoa maelezo ya namna ambavyo mashine inayotengeneza vipuri vinayoharibika ndani ya meli inavyofanya kazi kwa Naibu Waziri wa Wizara ya Uchukuzi, Dk. Charles Tizeba, alipotembelea Chuoni hapo Mwanzoni mwa wiki hii.
DSC_0724
Sehemu ya Menejimenti na wafanyakazi wa Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI), wakimsikiliza Naibu Waziri wa Wizara ya Uchukuzi, Dk. Charles Tizeba (Hayupo Pichani), wakati alipoongea nao mwanzoni mwa wiki.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Uchukuzi)

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

𝙂𝘼𝙈𝙊𝙉𝘿𝙄 𝙆𝘼𝘾𝙃𝙀𝙕𝘼 𝙆𝙄𝘽𝙄𝙉𝙂𝙒𝘼.