Wakamatwa wakiuza viungo vya binadamu

Kamishna wa jeshi Polisi katika mji wa Kwara nchini Nigeria Mr Ambrose Aisabor,amethibitisha kukamatwa kwa watuhumiwa wawili miongoni mwa wengine, waliokuwa wakijishughulisha na uuzaji wa viungo vya binadamu.
Akihojiwa na waandishi wa habari kamishna Ambrose alisema watuhumiwa Amos Kareem na Abubakar Ladan,walikamatwa kufuatia msako mkali ulio endeshwa na jeshi hilo na baada ya kuhojiwa kwa masaa kadhaa watuhumiwa walikiri kuhusika na tukio hilo.

Aidha kamishna Ambrose amesisitiza kuwa jeshi hilo bado linaendelea na uchunguzi ili kuwabaini watuhumiwa wengine.

Mmoja wa watuhumiwa, Abubakar Ladan, aliuambia mtandao wa Vanguard kwamba alikuwa ameahidiwa kupewa pikipiki kama angeweza kumpataia mteja wake kichwa, mkono na mguu wa binadamu. kwa mujibu wa mtuhumiwa , alidai kuwa nia ya yeye kufanya hivyo ni kutimiza ndoto yake ya kumiliki pikipiki hicho ndio kitu kilicho msukuma aende makaburini kufukua maiti na kukata kichwa,mguu na mkono kama inavyo onekana kwenye picha.

Mtuhumiwa wapili ambae ni Amos Kareem wakati akihojiwa alisema kuwa wateja wakubwa wa viungo hivyo ni wanasiasa na amesha wauzia mara nyingi,mtuhumiwa huyo alikataa kata kata kuwataja wanasiasa hao kwa majina kwa sababu za kiusalama dhidi yao.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*