Hatimaye
mshamabuliaji Geilson Santos Santana "Jaja" raia wa Brazil leo
amesaini mkataba wa miaka miwili (2014-2016) kuitumikia timu ya Young
Africans kwa ajili ya michuano mbalimbali ikiwemo ya Ligi Kuu ya Vodacom
pamoja na mashindano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika mwakani.
Katibu
mkuu wa Young Africans Bw Beno Njovu amesema usajli wa Jaja unakua ni
wa pili msimu huu kwa wachezaji wa kimataifa baada ya awali kumsajili
kiungo mshambuliaji Andrey Coutinho ambaye pia ni raia wa Brazil.
"Kazi
yetu uongozi ni kutekeleza maelekezo ya kocha mkuu pamoja na benchi la
ufundi, walitoa mapendekezo ya usajili kabla hawajaanza kazi na mengine
baada kuwasili yote tunajitahidi kuyatekeleza ili kila kitu kiende safi"
alisema Beno.
Jaja
ambaye alizaliwa tarehe 21 Septemba 1985 na kukulia katika mji wa
Aracaju nchini Brazili mpaka anasajiliwa na timu ya Young Africans
alikuwa akiichezea timu ya Itabaina FC iliyopo nchini Brazil.
Mshambuliaji
huyo mwenye mwili uliojaa vizuri tayari alishaanza mazoezi tangu
katikati ya wiki iliyopita chini ya Kocha Mkuu Marcio Maximo na msaidizi
wake Leonado Neiva ambao wanaendelea kukinoa kikosi cha Young Africans
kwa ajili ya michuano mbalimbali.
Comments