Amkata Kicwa Mdogo wake ili Apate Utajiri.....Aondoka nacho, Akipeleka kwa Sangoma.....Ilikuwa akiweke Dukani ili wateja Wafurike
Jeshi
la Polisi Mkoa wa Morogoro linamng’ang’ania mfanyabiashara maarufu wa
Wilaya ya Mvomero, Johnson Damian Mkude (39) akituhumiwa kumkata kichwa
mdogo wake wa kuzaliwa, Mathias kisha kuondoka nacho kwenda kwa mganga
kwa kile kilichodaiwa ni kufanyiwa dawa ili awe bilionea.
Tukio
hilo ambalo kwa sasa ndiyo gumzo mkoani Morogoro lilijiri usiku wa
Agosti 3, mwaka huu katika mashamba ya Kata ya Mlali ambapo ndugu wa
marehemu waliokuwa wakimsaka ndugu yao walifanikiwa kuona kiwiliwili
Agosti 6, mwaka huu.
Comments