MSANII wa muziki wa kizazi kipya Bongo, Baby Joseph
Madaha amenusurika kubakwa nchini Kenya baada ya kupanda jukwaani akiwa
ametinga kivazi cha nusu utupu.
Tukio hilo lilitokea Jumamosi iliyopita katika mji wa Naivasha uliopo
Nairobi nchini humo ambapo mwanadada huyo alipopanda jukwaani akiwa
amevaa sketi fupi iliyokuwa imeacha sehemu kubwa ya mapaja wazi, wanaume
wakware walianza kumvutia chini kwa…
MSANII wa muziki wa kizazi kipya Bongo, Baby Joseph
Madaha amenusurika kubakwa nchini Kenya baada ya kupanda jukwaani akiwa
ametinga kivazi cha nusu utupu.
Tukio hilo lilitokea Jumamosi iliyopita katika mji wa Naivasha uliopo
Nairobi nchini humo ambapo mwanadada huyo alipopanda jukwaani akiwa
amevaa sketi fupi iliyokuwa imeacha sehemu kubwa ya mapaja wazi, wanaume
wakware walianza kumvutia chini kwa nguvu.
“Nusura Baby Madaha abakwe, wanaume wakware walishindwa kuvumilia,
palepale jukwaani wakaanza kumvuta huku wengine wakimng’ang’ania paja
lake lakini aliokolewa na mabaunsa vinginevyo tungekuwa tunaongea
mengine,” kilisema chanzo.
Ijumaa limezinasa picha kadhaa zinazomuonesha Baby Madaha akiwa
anang’ang’aniwa na wanaume tofauti huku wengine wakimchungulia sehemu
zake ‘muhimu’ pamoja na kumshika mapaja yake.
“Kweli ilikuwa ni hatari siku hiyo maana wanaume waliniganda balaa
kila nilipokuwa naimba jukwaani walikuwa wakinivutia kwa huku chini
walikokuwa wamesimama lakini niliokolewa na mabaunsa, hata hivyo shoo
ilikuwa na mzuka sana,” alisema Baby Madaha.
Baby Madaha akipata akiwa na baadhi ya mastaa kutoka Kenya.
Kwenye shoo hiyo iliyokuwa na nyomi ya kutosha, Baby Madaha alikamua
vilivyo sambamba na wasanii wakali kutoka Kenya akiwemo Jua Kali na
Wayree.
Comments