MUIGIZAJI Jacqueline Pentezel maarufu kwa jina la Jack wa Chuz, amefunguka kuwa mume wake, Gadner Dibibi anapenda mwanamke mwenye mwili mkubwa yaani bonge.
Muigizaji Jacqueline Pentezel maarufu kwa jina la Jack wa Chuz
Akizungumza
na gazeti hili mwishoni mwa wiki iliyopita, Jack alisema isingekuwa
kuilinda ndoa, asingekubali auachie mwili wake aonekane bonge nyanya
kiasi hicho alichonacho hivi sasa.
Jacqueline Pentezel akiwa na mume wake, Gadner Dibibi
“Napenda
sana kumsikiliza mume wangu, chochote anachokihitaji nitakifanya hata
kama kipo nje ya uwezo wangu, nitajitahidi tu. Sasa alivyoniambia kuwa
anapenda mwili wangu uonekane wenye supu supu na minofu mingi nikakubali
ndiyo maana nimejiachia” alisema Jack.
Comments