MAULIDI KITENGE KUREJEA TENA HEWANI KESHO ATAKUWA NA PACHA WAKE KATANGA AMBAYE PIA AMEJIUNGA NA E FM
KITENGE WAKATI AKIKABIDHIWA MKATABA MPYA WA E FM. |
Mtangazaji mpya wa E FM Radio, Maulidi Kitenge anatarajia kuanza
kusikika tena hewani kesho Alhamisi.
Kitenge maarufu kama jezi namba 10 mgongoni anatarajia kuanza kusikika
katika kipindi kipya cha redio hiyo ambacho kitakuwa kikirushwa saa 1 usiku,
kila siku.
Akizungumza na SALEHJEMBE, Kitenge ambaye ni mtangazaji maarufu wa michezo nchini alisema wako katika maandalizi ya
mwisho kabla ya kuanza kipindi hicho saa moja kamili kesho Alhamisi.
“Maandalizi yanakwenda vizuri na Mungu akijaalia, Alhamisi tutaanza,”
alisema Kitenge.
Kitenge na mtangazaji pacha wake, Katanga wamehamia E FM wakitokea Radio
One.
Kitenge akifanya kazi Radio One kwa miaka 14 na siku nne zilizopita
aliaga rasmi na kuanza makazi mapya na redio hiyo mpya.
Comments