Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis kwa mara ya kwanza ametabiri hatima ya maisha yake duniani akisema kuwa anaamini Mungu anaweza kumpa muda wa miaka miwili au mitatu ya kuishi.Akizungumza na waandishi wa habari kwenye ndege wakati akitoka ziarani Korea Kusini kurejea Vatican, Papa Francis alisema suala la kuendelea kuishi ni neema ya Mungu.
alisema.Papa Francis (77), pia alizungumzia uwezekano wa kustaafu endapo atahisi kwamba afya yake hairuhusu kuendelea na kazi.
Utamaduni
wa kuachia madaraka ndani ya kanisa hilo linalotajwa kuwa na waumini
wengi duniani uliasisiwa upya mwaka jana na mtangulizi wake, Papa
Benedict XVI aliyeng’atuka kutokana na matatizo ya kiafya.Pamoja na
kwamba Papa Francis hajawahi kuzungumza hadharani kuhusu ni lini pengine
anaweza kufariki dunia, lakini baadhi ya vyanzo vya habari kutoka
Vatican vinasema kuwa kiongozi huyo amekuwa akiwaambia watu wake wa
karibu kuhusu siku zake chache zilizosalia duniani.
Wachambuzi
wa masuala ya kiimani kwa nyakati tofauti walisema huenda kiongozi huyo
ana tatizo la kiafya ambalo halijawekwa wazi.Wakati hayo yakiendelea
taarifa za ndani zinabainisha kwamba kiongozi huyo aliwahi kutolewa pafu
moja baada ya kuathirika wakati akiwa kijana nchini Argentina
Comments