Kamati
ndogo iliyoundwa kuchunguza tuhuma za upendeleo katika utoaji nafasi za
ajira 200 kwa watu waliyoomba nafasi hizo kupitia idara ya uhamiaji
imebaini kuwa nafasi hizo zimetolewa kwa upendeleo bila ya kufuatwa
taratibu, kanuni na sheria ya utoaji wa ajira hizo.
Akizungumza
na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, katibu mkuu wa wizara ya
mambo ya ndani ya nchi Mbarak Abdulwakil amesema kamati hiyo imeweza
kubaini kuwa mambo mengi yalifanywa kiujuma jumla sana na hivyo kutoa
mwanya wa watu kupindisha mambo.
Kamati hiyo iliundwa Agosti Mosi mwaka huu, chini ya watu watano ikiongozwa na yeye mwenyewe katibu mkuu wa wizara ya hiyo.
Iadha
katika mkutano huo jeshi la polisi kupitia mkurugenzi wa makosa ya
jinai kamanda Isaya Mngulu amesema jeshi hilo litafanya operesheni ya
kuhakikisha inawakamata na kuwafikisha mahakamani watuhumiwa wakiwemo
waganga wa kienyeji wanaojihusisha na vitendo vya kuwaua ama kuwajeruhi
walemavu wa ngozi kwa imani zao za kishirikina.
CHANZO: ITV TANZANI
Comments