SNURA KUPIGISHA KWATA LA 'MAJANGA' TARIME

NA MWANDISHI WETU
MWANAMUZIKI mahiri Tanzania na Afrika Mashariki katika mtindo wa mduara, Snura Mushi, anatarajiwa kutumbuiza kwenye Viwanja Vya Nyamongo, Rorya, onyesho ambalo linatarajiwa kuwa la aina yake.

Akizungumza kutoka Tarime, Mkurugenzi wa Taasisi ya Nyumbani Kwanza Media Group, Mossy Magere alisema msanii huyo atafanya onyesho baada ya maandamano ya Jumapili ya kupinga ukatili wa kijinsia.

Snura aliyvuma zaidi na kibao chake cha Majanga anatarajiwa kuwasili Rorya leo kwa ajili ya onyesho hilo.
Magere alisema lengo la maandamano hayo yatakayoongozwa na RPC wa Tarime-Rorya, Lazaro Mambosasa ni kuhamasisha jamii kuachana na ukatili dhidi ya wanawake.

Maandamano hayo yataanza saa 3:30 katika Hospitali ya Nyamongo na kuishia Shule ya Msinga Nyamongo.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI