Wakulima Mbeya Waneemeka na Elimu ya uzalishaji wa Mboga Mboga kutoka TAHA

Mh. Dr. Christine Ishengoma Mkuu wa Mkoa wa Iringa akipokea taarifa kuhusu mfumo wa taarifa za masoko kutoka TAHA unavyofanya kazi zake kutoka kwa Cyrila Antony Afisa wa Masoko
Mkuu wa mkoa wa Iringa  Mh. Dr. Christine Ishengoma akisikiliza maelezo kutoka kwa Mtaalamu wa kilimo wa TAHA Bw Ringo kuhusu uzalishaji wa zao la nyanya 
Elimu ikiendelea kutolewa
 Vitalu na green houses
 Aina Mbalimbali za matunda ambazo zimezalishwa na wakulima kutokana na elimu Bora waliyo ipata kutoka TAHA



 Mwananchi akipata maelezo kutoka kwa Mtaalamu wa TAHA
 Teknolojia ya umwagiliaji kwa mfumo wa kilimo cha matone ambao pia unaonesha utengenezaji bora wa matuta, nafasi na usafi
Hivi ni  Vitalu vya TAHA na Barton Tanzania
 Vitalu vya mboga na green house kama zinavyoonekana katika picha
 Watangazaji wa Radio Sweet FM ya Mbeya wakishangaa ubora wa karoti ambayo ni daraja la kwanza inapopelekwa sokoni
 Zao la chines
Zao la karoti lililopandwa kwenye vitalu vilivyopo ndani ya viwanja vya Nanenane Mbeya kwenye Banda la TAHA
 Mwananchi akifurahia maelezo kuhusu zao la karoti daraja la kwanza

********************
Wakulima na wananchi mkoani Mbeya wameendelea kuneemeka na elimu ya bure ya uzalishaji wa mazao ya mboga, viungo na matunda inayotolewa na Asasi ya wakulima, wafanyabiashara na watoa huduma ya mazao ya horticulture nchini Tanzania (TAHA).

Wakulima hao wameneemeka na elimu hiyo inayotolewa na maafisa wa ufundi wa kilimo kutoka TAHA kwa ushirikiano na wale wa Barton Tanzania ambao kwa pamoja wameweka kambi katika viwanja hivyo ili kuhakikisha jamii ya wakulima wa mboga kutoka ukanda wa Nyanda za Juu Kusini wanapata elimu ya msingi bora ya uzalishaji wa mboga wenye tija.

"Mpaka sasa tumetembelewa na wananchi na wakulima wasiopungua 460 ambao wamefika katika banda letu hapa Nanenane kwenye viwanja vya John Mwakangale wakitaka kujifunza mbinu na misingi ya awali ya uzalishaji wa mazao ya horticulture, hiyo ni ishara njema kwani inaonesha ni kiasi gani wananchi  wanatafuta mbinu fasaha inayoweza kuwakwamua kutoka katika uzalishaji wa mboga wa kawaida mpaka uzalishaji wa tija unaozingatia viwango vya kitaifa na kimataifa" Alisema Likati Thomas afisa Mawasiliano kutoka TAHA.
Akifafanua zaidi kuhusu elimu ya kilimo cha uzalishaji wa mboga kwenye banda la TAHA afisa mawasiliano huyo alisema kuwa wamepanda mazao tofauti katika ploti zilizopo kwenye eneo lao ambapo wakulima na wananchi wanaopata fursa ya kutembelea eneo hilo ujifunza teknolojia mbalimbali za uzalishaji kama vile uzalishaji unaozingatia Mbegu bora zenye tija.

Teknolojia nyingine ni pamoja na upandaji mazao unaozingatia nafasi kati ya miche na miche, umwagiliaji kwa njia ya matone(drip irrigation) unaozingatia uhifadhi wa maji na mazingira pamoja na ulimaji wa matuta yaliyoinuka ili kutoa nafasi kwa mizizi ya mimea kupenyeza kwenye udongo ili kujitafutia lishe.

Mbali na elimu hiyo ya uzalishaji wa mboga, wananchi wa Mbeya wanaotembelea banda hilo pia wanapata fursa ya kujifunza elimulishe kutoka kwa mtaalamu wa masuala ya lishe wa TAHA Bi. Lawrencia …..ambaye amekuwa akiwafundisha wananchi juu ya umuhimu wa ulaji wa mboga na faida zake kwa afya ya miili yetu.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI