CAMEROON MPYA YAIFUMUA IVORY COAST 4-1 YAYA TOURE NDANI, UGANDA YASHINDA MBIO ZA AFCON

Na Mwandishi Wetu, YAOUNDE
KIKOSI kipya cha Cameroon kimeendeleza wimbi la ushindi katika kuwania tiketi za Fainali za Mataifa ya Afrika mwakani Morocco, baada ya jana kuifumua Ivory Coast mabao 4-1 mjini Yaounde.
Clinton N'Jie na Vincent Aboubakar kila mmoja alifunga mabao mawili kwa Simba Wasiofungika huku bao pekee la Tembo wa Ivory Coast likifungwa na Mwanasoka Bora Afrika, Yaya Toure.
Aibu yao: Yaya Toure aliiongoza Ivory Coast jana ikifungwa 4-1 Cameroon iliyosukwa upya baada ya Kombe la Dunia  

MATOKEO KUFUZU AFCON JANA; 

Kundi A
Kongo 2-0 Sudan 
Afrika Kusini 0-0 Nigeria 
Kundi B
Malawi 3-2 Ethiopia
Algeria 1-0 Mali
Kundi C
Angola 0-3 Burkina Faso
Lesotho 1-1 Gabon
Kundi D
Cameroon 4-1 Ivory Coast 
Sierra Leone 0-2 DRC
Kundi E
Togo 2-3 Ghana
Uganda 2-0 Guinea
Kundi F
Cape Verde 2-0 Zambia
Msumbiji 1-1 Niger
Kundi G
Misri 0-1 Tunisia
Botswana 0-2 Senegal
Cameroon iliyosukwa upya baada ya Kombe la Dunia, ilishinda mechi ya kwanza ya Kundi D mabao  2-0 dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Jumamosi iliyopita.
Cameroon, Algeria, Kongo Brazzaville, Burkina Faso, Cape Verde, Senegal na Tunisia zimefanikiwa kushinda mfululizo mechi mbili za mwanzoni wakati Misri ina hali mbaya baada ya kufungwa mfululizo.
Mabingwa watetezi Nigeria wameendeleza rekodi ya kutofungwa na kuruhusu nyavu zao kuguswa na Afrika Kusini, baada ya kulazimisha nao sare ya bila kufungana 0-0 mjini Cape Town.
Super Eagles walipambana mno kupata sare hiyo ugenini, baada ya kupoteza mechi ya kwanza nyumbani mbele ya Kongo Jumamosi iliyopita.
Uganda imeifunga 2-0 Guinea, Algeria imeshinda 1-0 dhidi ya Mali mjini Blida, Kongo imeifunga Sudan 2-0 mjini Pointe-Noire, Burkina Faso imeichapa Angola 3-0 mjini Luanda na Cape Verde imewafunga mabingwa wa 2012 Zambia 2-1 mjini Praia.

Senegal imeshinda 2-0 dhidi ya Botswana mjini Gaborone na Tunisia imewafunga mabingwa wa kihistoria Misri 1-0 mjini Cairo, wakiwaacha Mafarao bila pointi katika Kundi G.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI