Neema
inazidi kumuangia Diamond Platinumz na leo amepata habari njema baada
ya kutajwa kuwania tuzo ya MTV EMAs huku akipokea tuzo kutoka nchini
Australia.Diamond
amewapa mashabiki wake habari njema za ushindi wa tuzo ya AAMA ya
Australia kupitia tiketi ya collabo ya aliyopewa na Desert Eagle, wimbo
unaoitwa ‘Everyday’.“Ningependa
niwajulishe kuwa kijana wenu nimepata tunzo nyingine toka Australia ya
Collabo bora ya Mwaka toka kwenye tunzo za #AAMMA_Awards kupitia nyimbo
niliyoshirikishwa na Desert Eagle iitwayo #EVERYDAY.
....
(jus wanted to inform you that, your favourite artist @Diamondplatnunz
won another award from Australia on #AAMMA_Awards as best Collaboration
song of the Year..).” Ameandika.
Wakati
huo huo, mtoto wa Tandale ametajwa kuwa moja kati ya wasanii wanaowania
MTV Europe Music Awards mwaka huu huku akichuana na wakali wengine
kutoka Afrika akiwemo Davido, Toofan (Togo) na Goldfish (Afrika Kusini).
Msanii
mwingine wa tano akisubiria kutajwa baada ya mashabiki kumpekeza kutoka
kwenye kundi la wasanii sita ambao ni Anselmo Ralph, Gangs of Ballet,
Mafikizolo, Sarkodie, Sauti Sol na Tiwa Savage.
Aidha, majina yote ya wasanii wanaowania tuzo hizo yatatajwa September 16 ambapo upigaji kura utaanza rasmi.
Hongera Diamond Platinumz, Tanzania inazidi kutajwa kwenye majukwaa ya
Comments