MC CHIMAMY POLE SANA DADA! UMETAFUTA MTOTO KUMBE UNAENDA KUFA DADA........



Jamani leo naona mitandaoni hii habari ya Msiba wa Mc Chimamy....

Inauma sana kuona wanawake tunapoteza Uhai wetu kwa sababu ya kuongeza au kuleta uhai wa mtu mwingine, kina mama tunazidi kuweka maisha yetu rehani kwa sababu ya kuongeza rasilimali watu.....yaani mwanamke akipata mimba anaanza kuingiwa na hofu ya kifo.... hata mie nilipokuwa mjamzito nilikuwa napata hofu sana sana.... siyo Haki hata kidogo....


Sitaki kulaumu lakini ifike mahali jambo hili la wanawake kufa kwa sababu ya uzazi lichukuliwe kwa umakini mkubwa na Serikali yetu.....

Mbona kuna nchi ambazo wanawake hawafi kwa sababu ya uzazi???? kwa nini wanawake wa Tanzania tunapuputika in the name of kuzaa?????
Takwimu za vifo vya kinamama kufa kwa sababu ya uzazi ziko juu.... ni lazima ifike mahali kinamama tukatae kufa kwa sababu ya kuleta rasilimali watu.... Ni Lazima serikali iamuke na kutuhakikishia uhai wetu kinamama....
Jamani dada Mc Chimamy Mungu ailaze pema roho yako wewe na mwanao mpz, ambae ulikuwa unamsubiria kwa raha zote....rip my love.....

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI