Bweni la
wanafunzi katika shule ya sekondari ya African Muslim iliyopo Laloleni
manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro linateketea kwa moto hivi sasa. Kwa
mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo wamesema moto huo umeanza majira ya
saa 2 za usiku huku chanzo chake bado hakijajulikana na ripota wetu
Dixon Busagaga aliye eneo la tukio anafuatilia ajali hii na atatujulisha
kila kitachojiri na kupatikana.
Kikosi cha zimamoto kimefanya jitihada za kuzima moto huo licha ya kukabiliwa na changamoto ya maji.CRDT MICHUZI BLOG
Comments