Rais Kikwete hawezi kutamka Bunge liahirishwe

      

Na Magreth Kinabo, Dodoma
Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba, ambaye ni  Mwenyekiti wa Kituo cha Demokrasia Tanzania(TCD)Mhe. John Cheyo amesema kwamba mchakato mzima wa Katiba utamalizwa kwa kura ya maoni ya wananchi, hivyo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt. Jakaya  Kikwete haiwezi kutamka leo kuliahirisha Bunge Maalum la Katiba kwa kuwa liko Kisheria.
Aidha Mhe. Cheyo alisema kilichoahirishwa ni mchakato wa kura ya maoni ya wananchi na si Bunge hilo kwa kuwa walikubaliana   katika kikao cha mashauriano, baina Rais Kikwete na  Viongozi  Wakuu wa Vyama vya Siasa vyenye wabunge vinavyounda TCD kuwa bunge hilo liendelee. 
Kauli hiyo imetolewa leo Bunge Mjini Dodoma na Mhe. Cheyo wakati wa mjadala wa kujadili sura zilizobakia za Rasimu ya Katiba Mpya, ambapo alisema hayo ndiyo makubaliano yaliyofikiwa.
 Aidha Mhe. Cheyo alisisitiza Katiba Mpya inayopendekezwa itakayopatikana itadumu kwa njia ya maridhiano.
“ Bunge hili linaendeshwa kwa mujibu wa sheria , Tangazo la  Serikali (Government Notice) Na 254 hili ndilo uhai wa Bunge hili hadi Oktoba 4, mwaka 2014, na wote tukakubaliana haiwezekani   Mhe. Rais akasema   leo Bunge likasitishwa.
“ Vitu viwili vikukutana  kwa nia ya maridhiano, vitu vingine vinaweza kuwekwa pembeni sawa na sasa na baadae vinaweza vinashughulikiwa kwa wakati huo,” alisema Mhe. Cheyo.
Mhe. Cheyo alisema anamwomba  Rais Kikwete atoe ruhusa ya kuwepo kwa kipindi maalum  cha kitakachorushwa na televisheni (video) ili kila mtu aonekana alichokisema, huku akionesha kusikitishwa na upotoshwaji wa makubaliano hayo, uliofanywa na baadhi ya wanasiasa.
 “ Mojawapo  ambayo tuliyokubaliana  Bunge hili lipate Katiba ambayo inapendekezwa na wananchi pia kwa hali tulinayo haiwezekani  mchakato mzima ukamalizika, mchakato utamalizika kwa kura ya maoni  ya wananchi. Kama tukifika  huko itabidi tuhairishe uchaguzi wa mwaka 2015.   Niliyoyasema  ndiyo makubaliano tuliyokubaliana,” alisisitiza.
Mhe. Cheyo alisema Rais Kikwete alikubali kukaa chini pamoja na TCD na hao wanaojiita Ukawa.
 Alisema  Rais Kikwete alifanya mazungumzo na  viongozi wa Vyama vya Siasa vyenye wabunge vinavyounda TCD  mara  kwa mara ya kwanza, Agosti 31, mwaka 2014 kwa saa nne na mara ya pili, Septemba 8, mwaka 2014 kwa  saa mbili. 
Kikao hicho cha mashauriano kilihusisha  kamati ya makatibu wakuu,  kamati ya wenyeviti wa vyama  vya CCM, CHADEMA,CUF na NCCR-  Mageuzi.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*