Sep
11
Mwezeshaji
wa Taasisi ya MAYEPS Tanzania Lucas Marco (wa pili kulia) akimpongeza
Mwenyekiti wa Taasisi ya MAYEPS Tanzania Rose Mang’enya wakati wa
uzinduzi wa kitabu kiitwacho “NITUNZE NIKUTUNZE FAINALI UZEENI” hivi
karibuni jijini Dar es salaam. Wa kwanza kushoto ni Meneja wa Taasisi
hiyo John Masumba na Afisa Habari Idara ya Habari MAELEZO Eleuteri mangi
(kulia).
Mwezeshaji
wa Taasisi ya MAYEPS Tanzania Lucas Marco (kulia) akizungumza na
waandishi wa habari (hawapo pichani) hivi karibuni jijini Dar es salaam
wakati wa uzinduzi wa kitabu kiitwacho “NITUNZE NIKUTUNZE FAINALI
UZEENI”, chenye maudhui ya kuwasaidia watu wanaofanyakazi ya kujiajiri
au kuajiriwa kufanya maamuzi yaliyosahihi ili waweze kuishi maisha bora
wakati wakiwa kwenye ajira na baada ya kustaafu. Katikati ni Mwenyekiti
wa Taasisi hiyo Rose Mang’enya na kushoto ni Meneja wa Taasisi hiyo John
Masumba.Picha na MAELEZO
……………………………………………………
BeatriceLyimo- MAELEZO
Taasisi isiyo ya kiserikali ya
MAYEPS Tanzania imezindua kitabu kiitwacho “NITUNZE NIKUTUNZE FAINALI
UZEENI”, chenye maudhui ya kuwasaidia watu wanaofanyakazi ya kujiajiri
au kuajiriwa kufanya maamuzi yaliyosahihi ili waweze kuishi maisha bora
wakati wakiwa kwenye ajira na baada ya kustaafu.
Akizungumza na waandishi wa habari
hivi karibuni jijini Dar es salaam, Meneja wa Taasisi hiyo John Masumba
amesema kuwa uzoefu unaonesha kuwa wafanyakazi katika jamii ya
Kitanzania hawaweki akiba kwa ajili ya kuwekeza kwa madhumuni ya kujenga
uchumi.
Meneja Masumba amesisitiza kuwa
MAYEPS imetambua kwamba ikiandaa warsha moja kwa mwezi juu wafanyakazi
kufanya maamuzi yaliyo sahihi, itawafikia watu 600 kwa mwaka.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa
Taasisi hiyo Rose Mang’enya aliwapitisha waandishi wa habari juu ya
yaliyomo kwenye kitabu hicho kwa kuendesha warsha fupi iliyowafungua
macho waandishi hao kuhusu namna ya kutunza fedha kuandaa maisha ya
baadaye.
Akinukuu kauli ya mtaalamu wa
uongozi John Maxwell Mwenyekiti huyo alisema kuwa “Watu wanaofanikiwa na
wasiofanikiwa hawatofautiani sana kiuwezo bali wanatofautiana katika
dhamira ya kufika kilele au upeo wa uwezo wao”.
Mang’enya aliongeza kuwa jukumu la
kujenga maisha binafsi lipo kwa muhusika binafsi, hivyo, watumishi
wawe na msimamo sahihi utakaowawezesha kuwa na maisha bora.
Aidha, MAYEPS hutoa mafunzo kwa wafanyakazi wa Umama na binafsi namna ya kupanga matumizi.
Pia hutoa mafunzo ambayo
yatawezesha wafanyakazi kutambua kuwa fedha za mafao au pensheni
hupungua thamani mwaka hadi mwaka hivyo uwekezaji wa fedha hizo ni
muhimu ufanywe kwa uangalifu.
Comments