UHAMIAJI KASUMULU YAJIPANGA KUDHIBITI EBOLA‏


Afisa Uhamiaji wa Kasumulu mpakani mwa Tanzania na Malawi, Elihuruma Mndeme akizungumzia hali halisi ya mpaka na maandalizi ya kukabiliana na ugonjwa wa Ebola.
 Barabara ya kuingilia Mpaka wa Kasumulu
 Hapa ni eneo la Tanzania kabla haujaingia katika Geti la Uhamiaji 
 Afisa Afya wa Mpakani Kasumulu, Ryoba Maijo  akielezea jinsi walivyojipanga kukabiliana na ugonjwa wa Ebola .
 Waandishi wa Habari wakiendelea kuchukua Taarifa Katika ofisi za Uhamiaji Kasumulu
 Shughuli mbalimbali zikiendelea upande unaounganisha Boda ya Tanzania na Malawi  
Afisa Uhamiaji wa Kasumulu mpakani mwa Tanzania na Malawi, Elihuruma Mndeme akionesha mpaka wa Tanzania na Malawi
 Hapa ni katikati ya Mpaka wa Tanzania na Malawi , Hapa waandishi wa habari  wakiuliza Maswali na kupata taarifa zaidi ya mpaka huo na Mwenyeji wao Afisa Uhamiaji wa Kasumulu mpakani mwa Tanzania na Malawi, Elihuruma Mndeme
Kikosi kazi cha Mbeya yetu Blog Kutoka kushoto ni Venance Matinya,Joseph Mwaisango na Fredy Anthony Njeje baada ya kazi kumalizika.
***********
WAKATI kukiwa na hofu ya kuingia kwa ugonjwa wa Ebola nchi jirani ya Congo, Maafisa uhamiaji mipakani wamejipanga kuhakikisha hakuna mgeni atakayeingia nchini akiwa na dalili za ugonjwa huo.
Hayo yalibainishwa jana na Afisa Uhamiaji wa Kasumulu mpakani mwa Tanzania na Malawi, Elihuruma Mndeme, alipokuwa akizungumza na Mbeya yetu  kuhusu mikakati ya kudhibiti wageni wanaoingia nchini kutokuleta ugonjwa huo.
Mndemi alisema yeye pamoja na maafisa wake wamejipanga kuhakikisha kila mgeni anayeingia nchini anakaguliwa vizuri kabla ya kuruhusiwa kuendelea na safari kwa kuangalia kama ana dalili zozote za Ebola.
Alisema ingawa bado hawajapelekewa vifaa maalumu vya kupimia wageni wanaoingia nchini ili kuwabaini kama wanazo dalili za ugonjwa huo lakini wanatumia mbinu mbali mbali kulingana na uzoefu walionao maafisa ikiwemo kumwangalia mtu na kumhoji.
Aliongeza kuwa hivi sasa Afisa anayegongesha stempu ni lazima ajiridhishe na maswali anayomuuliza mtu na sio kukimbilia kukagua hati yake pasipo kuangalia alikotoka na anakokwenda kama ndiko kuliko athirika na ugonjwa huo.
Alisema Mpaka wa  Kasumulu unachangamoto nyingi na kubwa ni kuwepo kwa njia za panya nyingi jambo linalowawia vigumu maafisa kudhibiti uingiaji holela wa wageni ambapo alisema kuna mipenyo 30 ya kuingilia nchini kutoka Nchi jirani ya Malawi.
Kwa upande wake Afisa Afya wa Mpakani Kasumulu, Ryoba Maijo,alisema  idara yake imejipanga kutokana na kuwepo kwa fomu maalumu ambayo mtu yeyote anayepita hapo atakuwa akijaza taarifa zake ambazo zitambaini kama ana maambukizi au hana.

Alisema tangu ugonjwa huo kuripotiwa baadhi ya Nchi idara hiyo imekuwa ikichukua tahadhari kubwa ili usije ukaingia nchini kupitia mipakani hivyo kuwa makini na kila mgeni anayepita hapo.

Na Mbeya yetu

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*