BABA ATELEKEZA MAPACHA HOSPITALINI BAADA YA MKE KUFARIKI MUDA MFUPI BAADA YA KUJIFUNGUA.

MWANAUME mmoja aliyejulikana kwa jina la Aison Majiyatamu mkazi wa Nankukwe Wilaya ya Chunya Mkoa wa Mbeya anatafutwa na uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mbeya kitengo cha Ustawi wa jamii kwa kutelekeza watoto wake Hospitalini.

Akizungumzia kisa hicho, Afisa Ustawi wa jamii, Hospitali ya Rufaa ya Mbeya, Annah Geretha, alisema wanalazimika kumtafuta mzazi huyo kutokana na kutoonekana Hospitali hapo kufuatilia maendeleo ya watoto wake kwa muda mrefu tangu walipozaliwa.

Alisema Mama mzazi wa watoto hao ambao ni mapacha wa kike aliyejulikanakwa jina la Edah Simia alifariki dunia muda mfupi baada ya kujifungua watoto hao salama kabisa ambapo mume aliuchukua mwili wa marehemu kwa lengo la kwenda kuzika kijijini kwao Namkukwe lakini tangu kipindi hicho hakuweza kurudi tena.

Alisema tukio hilo lilitokea Agosti 18, mwaka huu ambapo tangu kipindi hicho watoto wamekuwa wakihudumia na kuhifadhiwa kwenye chumba cha Joto katika Hospitali ya Wazazi ya Meta.

Alisema lengo la kuwatafuta ndugu wa watoto hao ni kutokana na muda wa kuendelea kukaa kwenye chumba cha joto umepitiliza kutokana na umri wao hivyo wanashindwa kuwatoa kwa sababu hawana mtu wa kuweza kuwahudumia nje ya Chumba hicho kutokana na uhaba wa wauguzi unaoikabili hospitali hiyo.
Alisema yoyote atakayekuwa na taarifa za ndugu wa marehemu ama baba wa watoto hao atao taarifa Hospitali ya Rufaa ya Mbeya au Hospitali ya Wazazi ya Mbeya kwa taratibu zingine.
Mwisho.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.